Habari za Punde

Wanahabari kutoka Afrika watakiwa kuwa chachu ya maendeleo kwa bara lao


Na Mwashamba Juma, Beijing, China

WANAHABARI barani Afrika wametajwa kuwa ni chachu ya kuibua na kuyatangaza mazuri yatokanayo na rasilimali na maendeleo ya bara hilo kwa kutumia kalamu na kamera zao sambamba na kuonesha uzoefu walionao kwa vyombo vya habari vya kimataifa ili kujenga uhusiano mwema katika kuimarisha kada ya habari barani humo.

Hayo yalielezwa na Naibu Mhariri Mtendaji wa gazeti la kila siku nchini China, “China Daily”, Gao Anming wakati akifanya mazungumzo na ugeni wa maaofisa na wanahabari kutoka mataifa 12 yanayozungumza Kiingereza barani Afrika walipotembelea ofisi za kazeti hilo mtaa wa Hu Xi, mjini Beijing.

Alisema ujio wa maofisa habari hao kwenye ofisi za “China Daily ni mwema wa kufungua chaneli za urafiki baina yao katika kubadilishana uzoefu ikiangaliwa gazeti hilo tayari limefungua milango na kuanza kusambaa kwa baadhi ya mataifa  barani Afrika.

 

Alisema mbali na hatua kubwa iliyofikiwa na “China Daily” ni mafanikio ya kusambaza gazeti hilo karibu kila pembe ya dunia katika kuifikia hadhira yake, aidha aliongeza kuwa, kuweza kufungua ofisi za kudumu na kuhakikisha gazeti hilo daima linasongambele na kukua kibiashara.


“Mbali na mafanikio ya “China Daily” lenye kurasa 26 lakini pia tunazalisha kopi za kila siku kwa “China Daily Hong Kong” (1997), Marekani (2009), Amerika Kusini (2012), gazeti la wiki barani Ulaya “China Daily European Weekly,” (2012), gazeti la kila wiki barani Asia (2010), Afrika (2012) na Latin Amerika (2013) ambayo yote ni watoto wa “China Daily” alifahamisha Naibu Mhariri huyo.

 

Alifahamisha barani Afrika “China Daily” lina makao kuu yake mjini Nairobi, Kenya na tayari limefungua ofisi Tanzania kwa upande wa Afrika Mashariki na kuongeza kuwa lengo la kuweka makao makuu ya gazeti hilo Kenya ni kwamba kiingereza kinazungumzwa sana nchini humo pia Nairobi, eneo lililobobea kibiashara. Hata hivyo Gao alisema mwakani “China Daily” linatarajia kufungua makao makuu yake nchini Misri na Nigeria.

 

Nae Mhariri Msaidizi wa China Daily, Ji Tao wakati akitoa ufafanuzi kwa maofisa na wanahabari hao alisema gazeti lao linajitahidi kuzalisha bidhaa zenye ubora kwenda sambamba na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

 

“Gazeti linajitahidi kuchapisha picha zenye ubora na contenti ya hali ya juu katika kuyafikia malengo tuliyojiwekwea, hii ni inatokana na ushindani wa teknolojia kwenye uzalishaji wa magazeti” alifahamisha.

 

Abel Plackie Afisa habari, Mkurugenzi masuala ya jamii, Wizara ya Habari Utamaduni na Utalii nchini Liberia, ambae pia ni mkuu wa msafara wa maofisa na wanahabari hao alisema mwaliko wa China Daily kwa wanahabari hao ni ishara na faraja njema katika kuunganisha nguvu moja na kubadilishana uzoefu baina yao.

 

“Tunajisikia faraja na wenye bahati kubwa kama wadau wa habari leo hii kuwa pamoja na wenyeji wetu, mbali ya kubadilishana uzoefu nanyi, hatua mliofikia ni ya kupigiwa mfano, napenda pia kutumia fursa hii kuishauri China Daily kuutumia ugenii huu kwa kuanzasha chaneli barani Afrika ili kukidhi haja ya malengo yake kwa Afrika.” Alishauri mkuu huyo.

 

Sambamba na kulishauri gazeti hilo jenga uhusianao na mitandao ya jamii kama “Face book na Twitta” katika kubadilishana mawazo na wanajamii kama moja ya vyanzo vya habari, kwani kwenye jamii kuna mengi yakuibua kama wanahabari.

 

“Mnaonaje mkatumia hii mitandaoo ya jamii katika kupata taarifa na kuweka habari zenu kwani kunakojamii kuna mengi na mnaweza kuibua mambo mengi. Alishauri.

 

Alisema “Chaina Daily” kusomwa dunia nzima kwa ulimwengu wa sasa ni mafanikio makubwa hasa katika kuitangaza China kwenye ulingo wa habari na uchumi dunuani kote.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.