Na Khamis Amani
MAHAKAMA Kuu
Zanzibar itasikilisha ombi la dhamana lililowasilishwa na mawakili wanaomtetea
aliewahi kuwa Waziri katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mansoor Yussuf
Himid, anayekabiliwa na mashitaka ya kupatikana na silaha na risasi 407.
Ombi hilo
litasikiliwa na Jaji Abraham Mwampashi
Agositi 11.
Juzi mahakama ya
mkoa Vuga chini ya Hakimu Khamis Ramadhan ilimnyima dhamana Mansoor baada ya
kufikishwa makamani hapo kujibu mashtaka matatu yanayomkabili.
Sababu zilizotolewa
na hakimu huyo ni kwamba shitaka la
kupatikana na silaha ni miongoni mwa mashitaka yasiyokuwa na dhamana kwa mujibu
wa kifungu cha 150 (1) cha sheria za mwenendo wa jinai (CPA) namba 7/2004 sheria
za Zanzibar.
Mahakama Kuu ndiyo
yenye mamlaka ya kisheria ya kutoa dhamana kwa makosa yote yasiyokuwa na
dhamana.
Ombi hilo
ameliwasilisha chini ya kifungu cha 150 (4) cha sheria za mwenendo wa jinai
(CPA) namba 7/2004 sheria za Zanzibar.
Mahakama Kuu tayari
imeshatoa hati za wito pamoja na hati ya kiapo iliyowasilishwa na mshitakiwa
huyo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ambae ndiye mpingaji wa dhamana.
Mansoor ambae
aliwahi kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya serikali na Chama cha Mapinduzi
(CCM) kabla ya kufukuzwa,anakabiliwa na mashitaka matatu ya kupatikana na
silaha, risasi na marisau kinyume cha sheria.
Silaha anayodaiwa
kupatikana ni bastola aina ya Bereta pamoja na mashitaka ya kumiliki risasi za
moto 295 za bastola na kumiliki risasi aina ya marisau 112 za bunduki aina ya
shortgun, badala ya marisau 50 alizoruhusiwa kisheria mashitaka ambayo yana
dhamana kwa mujibu wa sheria.
Kesi dhidi yake
inatarajiwa kufikishwa tena mahakama ya mkoa Vuga Agosti 18 mwaka huu kwa ajili
ya kutajwa, kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
No comments:
Post a Comment