Na: Ali Othman Ali
Shule
ya Msingi ya Wingwi Mtemani , Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, imepongezwa
na kuzawadiwa kwa kuweza kupasisha
wanafunzi 8 kati ya 46 waliofanya
mtihani katika awamu yao ya kwanza ya
mitihani ya darasa la saba mwaka 2013-2014 .
Tukio
la kuwazawadia Wazazi, Walimu na Wanafunzi wa shule hiyo limefanyika katika
hafla iliyoandaliwa na kudhaminiwa na Mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu
cha London, SOAS na Cambridge Bwana Yussuf Shoka katika viwanja vya shule hiyo
siku ya Jumamosi ya tarehe 30 Agosti, 2014.
Hafla
hiyo iliyosimamiwa na kuwakilishwa na mgeni mualikwa, Afisa wa Elimu Mkoa wa kaskazini
Pemba Bwana Muhammed Nassor Salim ilihudhuriwa pia na Wazazi, Wanafunzi na
Wanakijiji wa Shehia ya Mtemani ambapo Afisa huyo alimpongeza Bwana Yussuf
Shoka kwa moyo wake wa kizalendo na wa kujitolea kwa hali na mali hususan
katika nyanja ya Elimu hapa nchini.
Katika
hafla hiyo, Mwalimu Yussuf Shoka aliwashauri walimu kusimamia suala zima la
maadili na nidhamu kwa wanafunzi shuleni. Aidha, Bwana Shoka aliwataka
wanafunzi kusoma kwa bidii wakiamini kwamba Elimu ndio mkombozi wa maisha yao
na kwamba Elimu ni chachu ya maendeleo
ya taifa.
Wakati
huo huo Bwana Shoka amewazadia wanafunzi nane waliofaulu mchepuo darasa la saba
mwaka 2013, kwa kuwapa vifaa mbali mbali
vya kusomea na fedha taslimu za kujikimu.
Mwalimu
huyo pia ametoa fedha taslimu kwa walimu wote wa shule ya Wingwi Mtemani na
kamati nzima ya shule ya Msingi Mtemani
ili kuwapa motisha kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuendeleza
maendeleo ya Elimu na ustawi wa shule hiyo na Taifa kwa ujumla.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Bwana Shoka aliahidi kuipatia ofisi ya Mwalimu Mkuu kompyuta
moja, printer na mashine ndogo ya fotokopi kama zawadi kwa ajili ya shule hiyo.
Pia aliahidi kuanzisha maktaba ya kisasa katika shule hiyo ili kujenga na
kuendeleza utamaduni wa kusoma na kaundika ili kunyanyua kiwango cha Elimu na
ufaulu shuleni hapo.
Akihitimisha
hutuba yake kwa walengwa wa hafla hiyo, Bwana Shoka ameahidi kuendeleza
utamaduni wa kuwazawadia wanafunzi wote watakaofaulu katika ngazi ya mchepuo
kutoka katika shule zote nne za msingi
za Wingwi kuanzia mwaka 2015.
Aidha,
Bwana Shoka alibainisha sababu zilizompelekea kuandaa hafla hiyo kwa kusema;
‘Mimi si mwanasiasa, nabakia kuwa Mwalimu. Naomba nieleweke kuwa sitoi kwa
ajili ya kujijenga kisiasa na wala sitoi kwa sababu nina fedha nyingi. Natoa
kwa ajili ya Mungu, na kwa ajili ya ndugu zangu kwa kiasi ya uwezo niliojaaliwa
nikiamini kwamba kutoa ni moyo na wala si utajiri’.
Wakati
huo huo, Mgeni rasmi katika hafla hiyo Bwana Muhammed Nassor aliwaasa wanafunzi
kujiepusha na matumizi mabaya ya teknolojia ya kisasa ya internet na
Kompyuta kwa kuwataka wanafunzi wa shule
hiyo kuitumia teknolojia hiyo kwa ajili ya kujiendeleza na kujiletea maendeleo
yao na taifa kwa ujumla.
Ni mfano Mzuri wa Kuigwa ili Kuwatia mortisha watoto na Walimu waweze kufanya kazi kwa pamoja na kudumisha nidhamu. na kukaza kamba yakusoma... Kinachosikitisha nikwamba Wanafunzi wa Kiislamu hasa Wenye Majina ya Kizanzibari huanza vizuri huku Chini hata Wakifika Form 4 na Form 6 Wakafelishwa na kupata FFFFFFFF tupu..
ReplyDeleteKwasababu Wazanzibari bado Tunatawaliwa na Mkoloni Mweusi Tanganyika ambae anamiliki hata Baraza la Mitihani... Na Ikiwa SMZ itaendelea Kushikiliwa na Ngedere Wasiokua na Vission isipokua Kujaza Matumbo yao tu na Fitna.. Basi Juhudi za wanafunzi hawa na walimu wao Zitaishia Ukingoni.