Na Joseph
Ngilisho,Arusha
WASHTAKIWA wa
kesi ya ugaidi na kusajili vijana kujiunga kundi la Al- Shabaab la Somalia, wameutaka upande wa Mashitaka
kuwaeleza alipo mshitakiwa mwenzao namba mbili, Abdallah Thabit.
Malalamiko
hayo waliyatoa jana mbele ya Hakimu Mkazi ,Rose Ngoka, wakati kesi hiyo
ilipotajwa na kuiomba mahakama iwaeleze alipo mwenzao ambaye walikamatwa naye
pamoja.
Swali hilo
liliulizwa na mshitakiwa Ally Hamis
ambaye alinyoosha mkono na kumuomba Hakimu Ngoka kwa kusema kuwa ni muda mrefu
umepita tangu walipokamatwa lakini
wanashanga mshitakiwa mwenzao Thabiti kutomwona
mahakamani.
Alisema
walikamatwa na mwenzao Thabiti lakini tangu wapandishwe kizimbani kwa mara ya
kwanza Julai 24,hadi leo hii hajaletwa mahakamani.
Akitoa taarifa
mbele ya mahakama hiyo, Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Gaudencia Joseph
alidai kwamba ndio mara yake ya kwanza ameisikia taarifa hiyo hivyo atakwenda
kuifanyia kazi.
“Taarifa hii
ndio naisikia leo hapa na hii ni kwa sababu Mwendesha Mashitaka anayesimamia
shauri hili leo hayupo, hivyo sikuwa na taarifa kama walishawahi kuwasilisha
malalamiko yao na yeye atakapokuja siku nyingine atasema huyo mtuhumiwa yupo
wapi,” alidai.
Alisdai upelelezi
wa shauri hilo
bado haujakamilika hivyo kesi hiyo iahirishwe hadi tarehe nyingine.
Hata hivyo
Hakimu Ngoka aliingilia kati na kutoa ufafanuzi kwamba majibu sahihi yangeweza
kutolewa na Mwendesha Mashitaka aliyekuwepo kwani hata Hakimu anayesikiliza
shauri hilo
naye hakuwepo.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 3 mwaka
huu huku.
Washtakiwa
wanakabiliwa na kesi ya ugaidi, ambapo sheria namba 22 ya mwaka 2002 inasema
upelelezi ukishakamilika, mahakama kuu ndiyo yenye mamlaka ya kuisikiliza na
kutoa uamuzi.
Washitakiwa
hao wanakabiliwa na mashitaka ya kuua, kujaribu kuua, kusajili na kusafirisha vijana
kujiunga na Al-Shabaab.
Mbali na
mashitaka hayo pia wanahusishwa na tukio
la mrpuko wa bomu lilitokea baaya
Arusha Night Park jijini Arusha na kusababisha kifo cha mtu mmoja na
kujeruhi wengine 16.
Washitakiwa
hao ni Abdallah Athumani, Abdallah
Thabiti,Ally Hamisi, Abdallah Wambura, Rajabu Hemedi, Hasani Saidi, Ally
Hamisi, Yasini Sanga, Shaabani Wawa,Swalehe Hamisi,Abdallah Yasini, Abdallah
Maginga na Sudi Nasibu Lusuma.
Wengine
walioongezwa katika shauri hilo ni Shaban Musa, Athuman Hussein, Mohamed Nuru,
Jafari Lema, Abdul Mohamed na Said Michael Temba.
No comments:
Post a Comment