Habari za Punde

Vitambulisho vya NIDA vyasifiwa

Na Amina Omari, Tanga
UAMUZI wa serikali kuchagua teknolojia ya SMART CARD kutumika katika vitambulisho vinavyozalishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) umeipa Tanzania sifa kubwa barani Afrika.

Hayo yalibainishwa na Mkurungezi wa Mifumo ya Teknolojia ya Habari kutoka (NIDA), Joseph Makani, wakati akisoma hotuba kwa niaba ya  Mkurungenzi Mkuu, wakati wa uzinduzi wa zoezi la usajili na utambuzi wa watu mkoa wa Tanga.

Alisema hatua hiyo itasaidia taifa na watu wake kuleta mabadiliko makubwa katika nyanja za kiuchumi, kijamii kutokana na kuwepo kumbukumbu za taarifa sahihi kuhusu hali zao.

Aliwaomba watendaji kuhakikisha wanawajibika ipasavyo kuhakikisha zoezi la usajili na utambuzi kwa mkoa wa Tanga, linafanikiwa kwa ufanisi.


Nae Mkuu wa mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, aliwataka viongozi kuwapatia maelezo muhimu watendaji wa mitaa, vijiji na kata kuhusu namna bora ya ujazaji wa fomu za vitambulisho. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.