Kikosi cha timu ya Kombaini ya Makipa wanaoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja baaada ya mchezo wao na timu ya Waandishi wa habari za michezo Tanzania TASWA.
Kikosi cha timu ya waandishi wa habari za michezo Tanzania TASWA wakiwa katika picha ya pamoja
Na: Mpalule Shaaban
Kampuni ya Twiga Cement ya jijini
Dar es Salaam, jana imefanikiwa kuzindua rasmi Chama cha Wachezaji wa Nafasi ya
Golikipa wanaoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania, ambapo katika uzinduzi huo
timu hiyo ya Makipa ilicheza mchezo wa Kirafiki dhidi ya Timu ya Kombaini ya
Waandishi wa Habari TASWA F.C.uliofanyika kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama
jijini Dar es Salaam jana.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na
Ushindani wa Kipekee kutokana na Timu zote kuwa na Wachezaji Nyota na Tegemeo
katika Vipaji vyao, Mashabiki waliofika kushuhudia mchezo huo walifurahishwa na
jinsi kila mchezaji alivyoonyesha Ujuzi binafsi na kiwango cha hali ya juu.
timu ya makipa ndiyo iliyokuwa ya
kwanza kufanya shambulizi kwenye lango la timu ya TASWA ambapo dakika ya 26
mchezaji Shaaban Kado alikosa Penalt kutokana na beki wa Taswa Martin Peter
kunawa akiwa eneo la kumi na nane na penalt hiyo ilidakwa na kipa nyota wa
TASWA Ahmed Famau.
hadi kipindi cha kwanza kinamalizika
kikosi cha timu ya Makipa kilikuwa mbele kwa bao 1-0,lililofungwa na Juma
Kaseja baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa TASWA, ambapo kipindi cha
pili kila timu ilifanya mabadiliko ambapo Taswa iliwatoa, Majuto Omary, Ibrahim
Masoud, Ally Mkongwe, Zahoro Mlanzi, Shafii Dauda, na nafasi zao kuchukuliwa na
Salum Jaba, Juma Ramadhani, Hatibu Naheka,na Paul Limoy,mabadiliko ambayo hata
hivyo yalishindwa kupunguza kasi ya wachezaji hao Makipa wa Ligi kuu waliokuwa
muda wote wakilisakama lango la TASWA FC.
pamoja na kuwa na wachezaji wa akiba
timu ya Makipa lakini walishindwa kufanya mabadiliko, kutokana na wachezaji wengi
kuwa na pumzi ya kuwamudu TASWA ambapo Makipa hao walisaidiwa na mlinda mlango
kutoka timu ya Taifa ya Wanawake Twiga Stars, Fatuma Omary ambaye hata hivyo
alionyesha kiwango kikubwa baada ya kudaka michomo ya wazi kutoka kwa
washambuliaji wa Taswa,Ibrahim Masoud, Shafii Dauda,Majuto Omary pamoja
na Ally Mkongwe waliokuwa wakilisakama Lango la timu ya makipa kila wakati.
goli la pili lilipatikana kunako
dakika ya 67 kupitia kwa Ivo Mapunda aliyefunga kwa shuti kali lililomshinda
mlinda wa TASWA Ahmed Famau,kabla ya shaaban Kado kuhitimisha Kapu la
Magoli kwa timu hiyo ya Makipa.
Pamoja na Kufungwa kwa Taabu
3-0 timu ya TASWA FC, iliweza kuwachezesha mputa mputa wachezaji hao nyota wa
Ligi kuu pamoja na kwamba wachezaji hao muda mwingi wanakuwa kwenye Mazoezi
Makali na Timu zao za ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara,kitendo ambacho
kiliwafanya kuonekana wakiwa na Uhai wa kukimbiza huku na kule katika kipindi
cha dakika zote za mchezo.
Taswa ambayo kwa asilimia kubwa
iliwachezesha wachezaji wake wengi ambao ni wafanyakazi wa vyombo mbali mbali
vya habari, ilisifiwa na mashabiki waliohudhulia mchezo huo kwa kuwa Muda
mwingi wanakuwa katika shuguli za kiofisi ambapo kwa mujibu wa Mwenyekiti wa
Timu hiyo wachezaji ukutana mara moja kwa wiki kwa ajili ya mazoezi ya Pamoja.
"timu yetu ni nzuri sana hii
TASWA, mwenyewe umeona wachezaji walivyowapeleka mpuata hawa Makipa pamoja na
kwamba hii timu ya Makipa ni Wachezaji wa ligi kuu, nasema ligi kuu kwa kuwa
wanashiriki hiyo ligi isipokuwa tofauti wao ni makipa, na tunapozungumzia suala
la Wachezaji, mwenyewe unajua timu ili iwe bora ni lazima kwanza iwe na Makipa
wazuri ndipo iwe bora, na kipa bora ni yule anayeweza kuwapanga wachezaji wake,
hivyo kama hawa wachezaji ndiyo wapangaji wa timu zao wakati wa Mashindano,
mimi nasema tumecheza na Timu ya Taifa na si kama unavyofikili wewe, na ndiyo
maana nathubutu kusema kuwa kufungwa kwetu mabao 3-0 ni sawa na kupata ushindi
sisi, maana hata hivyo wametuleta kwenye Uwanja wao, nadhani wakati wa mchezo
wa Marudiano bila shaka itakuwa zamu yetu kuibuka na ushindi maana leo
wameshinda wao na mpira ni mchezo wa mmoja kushinda, asiyekubali kushindwa siyo
mshindani" alisema majuto
na kuongeza kwamba mchezo huo kwa
pande zote mbili umewapa changamoto ya kuifanya sasa timu hiyo ya Kombaini ya
Makipa kutambuliwa kote Nchini.
"mkakati uliopo sasa ni
kuhakikisha kwamba timu hii inazunguka kwenye Majiji Makuu kwa ajili ya kufanya
michezo yake ya kirafiki na timu za Mikoa, lakini lengo kubwa ikiwa ni kuwapa
Fursa wakazi wa Maeneo hayo kuwatambua zaidi hawa Makipa wetu, lakini pia
wakati wachezaji hawa wakiwa kwenye hayo maeneo ya Majiji watakuwa na jukumu la
kuwaandaa wachezaji wengine zaidi vijana katika nafasi za kipa ili kuweza kuwa
na Makipa wengi zaidi kwa ajili ya Faida ya Taifa letu la Tanzania"
alisema Majuto
Naye kocha wa Taswa FC Ally Mkongwe
wakati akizungumza na wachezaji wa timu zote alisema kuwa ni jambo la
kufurahisha ambalo limeweza kufanikiwa kwa asilimia 100 kwa kuwa lengo ilikuwa
ni kufanya uzinduzi na timu zote zimeweza kucheza kwa hali kubwa bila vurugu
wala kuonyeshana mchezo mbaya.
"tumefurahi sana, niwapongeze
wachezaji wote yaani Makipa na Taswa, jambo hili si la mzaha kama tulivyofikili
hapo mwanzo, lakini kumbe mwitikio wa watazamaji ulikuwa ni mkubwa sana na
wengi wamekuja kuwatazama wachezaji na Waandishi wa habari, Watangazaji, na
wakati umefika tukae tuangalie namna ya kuboresha mahusiano haya yawe ya kudumu
baina ya TASWA na timu hii ya Kombaini ya Makipa wa Ligi kuu, isipokuwa
tusameheane kwa yale Mapungufu madogo yaliyotokea maana sisi ni binadamu lakini
wakati mwingine nadhani hayatatokea kwa pande zote mbili endapo yametokea kwa
mchezo wa leo" alisema Mkongwe.
Hata hivyo wachezaji hao Makipa
wametakiwa kufanya jitihada za kuhakikisha wanakuwa chachu ya kuleta Makipa
wengine nyuma yao kutokana na kwamba nafasi ya Makipa kwa Tanzania inazidi
kupungua kutokana na nafasi hiyo kuwa ngumu ukilinganisha na nafasi za
wachezaji wengine wa ndani ambao wanakuwa ni wengi.
Naye mmoja wa Makocha wasaidizi wa
timu ya TASWA Ibrahim Masoud aliwaasa wachezaji hao kuwa kioo kwa wenzao na
kuwa kishawishi cha kuwapata vijana wengine watakaokuwa makipa wa Tanzania
miaka ijayo"Sina Mengi ya Kusema kwa kuwa Kocha na Mwenyekiti wameeleza
kwa kirefu lakini mimi niko tofauti kidogo na wenzangu, kikubwa hapa mimi ni
kuhusu nyie Makipa wetu, kumbukeni kwamba nyinyi kina Kaseja, Ivo Mapunda,
Shaaban Kado, Dida, mstafa na nyinyi wote, nyie sasa mnaelekea Ukingoni, ni
kama kina Mwameja wakati wao, kina Manyika, Mfaume,nk, walikuwapo lakini
walipopotea hao makipa Tanzania iliyumba sana kuwapata nyinyi, na hiyo
inatokana na kwamba Wachezaji wengi Makipa hawapati Fursa ya kuandaliwa, na
niwatake sasa kutumia mwanya huu kwa kuwa tayari mmekuwa ni makipa Hodari
kuhakikisha kwamba wakati wa Mapumziko ya Ligi, muweze kuingia Darasani kwa
ajili ya kupata ujuzi wa kuwa Walimu wa Makipa, Kila mmoja kwa wakati wake
lengo mtakapomaliza muda wenu wa kuitumia Tanzania katika Soka, muweze kuwa
walimu wazuri na wazalishaji wazuri wa Makipa wengine" alisema Ibrahim
Masoud(Maestro)
Kwa Upande wao Makipa hao wao
hawakuwa na la kusema isipokuwa kwa niaba ya wachezaji wote wa Makipa Ivo
Mapunda alisema kuwa wanashukuru kwa Sapoti kubwa kutoka Chama cha TASWA, ambao
mara zote wamekuwa mstari wa mbele kuwapa maelekezo, kitendo kilichowaweka
karibu zaidi hata wakati wa Uzinduzi wa Chama hicho cha Magolikipa," Sisi
binafsi tumefurahi kukutana na timu hii ya TASWA, maana kiujumla wachezaji
wengi wa Taswa wanafahamu mpira, ila tumewafunga kutokana na kukosa Pumzi
tofauti na sisi wengi tunafanya mazoezi kila siku na timu zetu tena timu kubwa
za ligi kuu, mimi Kesho( Leo) naelekea Zazibar Kambini, kujiunga na Timu yangu,
kwa hiyo unaona jinsi mchezo huu ulivyokuwa ni muhimu sana kwetu hata nimeshindwa
kuongozana na wachezaji wazangu pamoja na Mwalimu wangu kutaka nisicheze hii
leo lakini nimemkatalia kwamba ni lazima nijumuike na Makipa wenzangu kwenye
jambo hili la Umoja, maana sasa sisi Makipa pia tumekuwa ndugu wa karibu na
Marafiki wa Kweli, zama za kale kwamba huyu na huyu aziivi eti kwa kuwa wote ni
Makipa imepitwa na wakati, utatukuta mimi, Kaseja, Kado, Dida, Mstafa, na
wengine tukizungumza na kufurahi pamoja, sisi siyo maaduni ni marafiki tena
niwapongeze Wadhamini wa Mpambano huu(Uzinduzi) Kampuni ya TWIGA CEMENT kwa
kufanya jambo hili, limezidi kutuweka karibu zaidi, na naamini kwamba watazidi
kutuunganisha na kuandaa michezo Mingi zaidi kwa ajili ya kuwapa Raha wakazi na
mashabiki wetu Mikoani" alisema Ivo Mapunda
Akizungumzia
mchezo huo Afisa Masoko wa TWIGA CEMENT,Alex Gideon, alisema kuwa
maandalizi yamekwenda kama walivyopanga isipokuwa mkanganyiko umetokea kwenye
eneo dogo la Uwanja, ambapo awali mchezo huo ilikuwa ufanyike kwenye uwanja wa
KARUME kwa mujibu wa Matangazo yaliyofanywa na vyombo vya habari,
"
sitaki kulizungumzia sana suala la mkanganyiko wa Uwanja, lakini nadhani TFF
katika hatua za mwisho imeshindwa kuruhusu mchezo wetu kufanyika kwenye viwanja
vyao ambako vyombo mbali mbali vilitangaza, hivyo mashabiki wengi walifika
Karume, na nichukue fulsa hii kuwataka radhi sana wote waliotufuata kwenye
viwanja vya Karume, mchezo wetu ulibadilishwa uwanja kutokana na sababu
zilizokuwa nje ya uwezo wetu na kwa kuwa ni TFF wenyewe waliopanga hatua za
Mwisho Mchezo wa Ligi daraja la kwanza kufanyika humo hatukuwa na kipingamizi,
ni jambo la kimchezo na ukizingatia ni ligi yetu pia sisi watanzania hivyo hilo
niombe radhi kwa mashabiki wetu wote, lakini kuhusu wadhamini wetu kama
ulivyoona mwenyewe wamejitaidi na huu ni mwanzo na maandalizi yamefanyika kwa
siku chache zana, wakati ujao tutaboresha na kulifanya jambo hili kuwa la
kudumu na lenye kuleta tija ya Maendeleo kwa hawa Makipa wetu, kingine
niwapongeze TASWA kwa ushirikiano wao maana wametufariji na kutupa sapoti
kubwa"
alisema
Alex Gideon
aidha mchezo huo ulikuwa kwa ajili ya kujenga mahusiano mema
baina ya timu zote, wachezaji pamoja na kufanya Uzinduzi wa Chama cha Makipa
Tanzania, waandishi na Makipa wanaocheza ligi kuu Ya Vodacom Tanzania.
No comments:
Post a Comment