Na Mwandishi wetu
Kamanda wa Polisi Wilaya ya
Kati, Maulid Khamis, amelazwa hospitali kuu ya Mnazi Mmoja akitibiwa majeraha
aliyopata baada ya kugongwa na gari katika eneo la Mtoni wilaya ya magharibi
Unguja.
Kamanda huyo amelezwa eneo la
Mapinduzi Kongwe katika hospitali hiyo baada ya kupata majeraha sehemu ya usoni
na mguuni.
Kwa mujibu wa polisi, Kamanda
Khamis, aligongwa na gari yenye namba za usajili Z 591BN iliyokuwa ikitokea
Amani kuelekea Mtoni wakati Kamanda huyo akiendesha vespa yenye namba Z591DQ.
Dereva wa gari hiyo ambae
alikimbia baada ya ajali, alimgonga kwa nyuma wakati akitokoea Amani kuelekea
Mtoni.
Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo
kasi wa dereva wa gari huku akishindwa kuchukua tahadhari.
No comments:
Post a Comment