Habari za Punde

Ustadh alielawiti mwanafunzi wake aongezewa miaka 15 jela

Na Khamisuu Abdallah
Mwalimu madrasa ya Kadiria iliyopo Amani mjini Zanzibar, Hamad Bakar Mohammed, anaetumikia kifungo cha miaka 15 jela kwa kosa la kumlawiti  mwanafunzi wake wa kiume, ameongezewa adhabu nyengine ya miaka 15 jela na Mahakama ya Rufaa Tanzania.

Hukumu hiyo ilikuja baada mshitakiwa huyo kupinga kifungo cha miaka 15 alichopewa na Mahakama Kuu Zanzibar baada ya upande wa mashtaka kupinga uamuzi wa mahakama ya Mkoa Vuga, kumuachia huru mshitakiwa.

Adhabu hiyo ilitolewa na Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar,Abdul- hakim Ameir Issa.

Uamuzi wa kumuachia huru mshitakiwa huyo katika mahakama ya Vuga, ulitolewa na Hakimu Makame Mshamba Simgeni, baada ya kusema ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka hautoshi kumtia hatiani.


Jopo la majaji watatu akiwemo Jaji Kimano, Jaji Njasiri na Jaji Luonda, walitupia mbali rufaa ya mshitakiwa kupinga kifungo hicho na badala yake ikaamua kumuongezea kifungo chengine cha miaka 15.

Adhabu hiyo mpya sasa inamfanya mshitakiwa huyu kutumikia kiufungo cha miaka 30 jela.

Wakitoa hukumu majaji hao walisema vitendo hivyo vimekithiri licha ya kukemewea na Serikali na kwamba adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.


Hukumu hiyo ilitolewa Februari 13 mwaka huu huku upande wa mashtaka ukiwakilishwa na Maulid Ame Mohammed kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka.

2 comments:

  1. Hii safi sana maana hawa watu wamekuwa wabaya kuliko hata wanyama kazi yao kuharibu watoto wawatu nimefurahi sana kwa adhabu hii

    ReplyDelete
  2. Kama itaendelea kuwa hivi katika utoaji wa adhabu huenda ikatusaidia na kuleta usalama kwa watoto wetu. Hongera majaji kwa kutoa funzo kwa wengine

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.