Ali Issa Maelezo- Zanzibar
Hakuna sababu itayoifanya Zanzibar kushindwa kuitumia lugha ya Kiswahili katika kufundishia wanafunzi Skuli kwani Zanzibar ina hazina kubwa ya watalamu na ndio chimbuko la Kiswahili katika Nchi za Afrika na Dunian kwa ujmlai.
Hayo yamesemwa leo huko Eacrotanal Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Mohamed Seif Khatib wakati wa ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani yalio fanyika hapo.
Amesema inawezekana kabisa na frusa hiyo ifanyiwekazi kwa kukaa pamoja Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar pamoja na Wizara ya Habari UtAMADUNI Utalii na Michezo Zanzibar kuzipitia sera zilizo tangulia kulipatia mamuzi suala hilo.
Amesema kunanchi nyingi tu duniani ambazo zinasomeshwa kwakutumia lugha zao na haijawa tatizo katika nchihizo.
“Kuna nchi kama China,Uholazi na nyengnezo wanatumia furusa ya kusomeshea wanafunzi kupitia lugha zao,”
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khadija Bakar na Naibu Katibu Mkuu Wiara ya Habari, Utamaduni,Utalii na Michezo Zanzibar Issa Mlingoti alisema watakaa pamoja na wizara zao kulijadili suala hilo kwani hadi sasa kuna sera mbilizo pingana.
Wamesema wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wao wamelikubali hilo kuwa wanafunzi wafundishwe kupitia lugha ya Kiswahili la kini Wizara ya Elimu wao wanalipinga,hivyo watakaa pamoja na kusawazisha ili waendesambamba na wezao wa Tanzania Bara.
Nae Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) pia mjumbe wa baraza la kiswahili Zanzibar Mmanga M. Mjawiri amesema kuna umuhimu mkubwa wanafunzi Skuli wafundishwe kupitia lugha yao ya kishwahili kwani kiengereza Tanzania bado kikwazo.
Hakuna masiliano mazuri kati ya walimu na wanafunzi wakati wa kufundisha hivyo Kiswahili ndio suluhisho la wanafunzi kumuelewa mwalimu.
No comments:
Post a Comment