Habari za Punde

Mama Mwanamwema Shein Awafariji Waliopata Maafa ya Mvua Kituo cha Mwanakwerekwe Zanzibar.

Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif, wakiwatembelea Wananchi waliohifadhiwa katika Kambi maalum iliofunguliwa katika Skuli ya Mwanakwerekwe Unguja wakipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kambi hiyo Afisa Mdhamini wa Idara hya Maafa Zanzibar Bi Hamida Mussa.

WAananchi waliopata maafa wakiwa katika kambi maalumu iliotengwa kwa ajili yao, katika skuli ya sekondari ya mwanakwerekwe C,kuishi kwa muda katika kambi hiyo,
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akizungumza na Wananchi wanaoishi katika kambi ya Mwanakwerekwe Unguja baada ya nyumba zao kujaa maji kutokana na Mvua. Kulia Mke wa Makamu Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif na kushoto Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Dk Khalid Salum.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Dk Khalib Salum, akitowa maelezo ya kambi hiyo ya Wanaoishi Wananchi waliopata Maafa ya Mvua za Masika zilizonyesha hivi karibuni na kuleta madhara kwa familia mbalimbali kukosa pa kukaa.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe Abdallah Mwinyi Khamis, akizungumza wakati wa ziara ya Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kuwatembelea na kuwafariji na kutowa misaada ya Kijamii kwa Wananchi hao. 
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif, akizungumza na kuwafariji Wananchi waliopata Maafa ya Mvua wakati wa ziara ya Mama Mwanamwema Shein, na Ujumbe wake wa Wake wa Viongozi wa CCM Wabunge na Wawakilishi. 
Wananchi waliopata maafa wakiwa katika kambi maalumu iliotengwa kwa ajili yao katika Skuli ya Sekondari ya NMwanakwerekwe  C,  Zanzibar ,wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akipofika kuwafariji na kutowa misaada kwa ajili yao.
Mmoja wa Mwananchi wa Kwahani Bi Manaharusi Mwinyi, akitowa shukrani kwa niaba ya Wananchi waliopata maafa wanaoishi katika kambi hiyo akitowa shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar na Ujumbe wake wa Wake wa Viongozi  wa Wawakilishi na Wabunge waliofika katika kambi hiyo kuwafariji kwa maafa hayo.
Mmoja wa Wananchi waliopata mafaa ya Mvua za Masika zilizonyesha hivi karibuni katika maeneo ya Zanzibar akisoma dua baada ya kumalizika kwa hafla hiyo.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akimfariji na kumpa mkono wa pole Ndg. Suleiman Ramadhani,  kwa kufiwa na ndugu yake Haji Habibu, wakati  wa maafa ya mvua za masika.


Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akimkabidhi kiti maalum (wheel chair) Bi. Fathiya Rashid, kwa ajili ya mzee wake Bi Safia Omar ni mmoja wa mwananchi alieathirika na mvua katika maeneo ya kwahani Unguja.kushoto Mkuu wa Wilaya ya Magharibi Mhe Ayuob Mohammed Mahmoud.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akimkabidhi Kanga Afisa Muandamizi  Idara ya Maafa na Mkuu wa Kituo cha Waathirika wa Mvua Bi Hamida Mussa. Kwa ajili ya Wananchi wa kituo hicho.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.