Aliyekuwa Wanachamna
wa CUF na Mbunge wa jimbo la Wawi kisiwani Pemba, ambaye kwa sasa amehamia
chama cha ADC, Hamad Rashid Mohamed leo amechukuwa fomu ya kugombe urais wa
Zanzibar kupitia chama cha ADC, kulia ni kamishna wa ADC kanda ya Pemba Saidi
Seif akimkabidhi mgombe huyo Fomu
MGOMBEA urais wa
Zanzibar kupitia Chama cha ADC, Hamad Rashid Mohamed katitaki akizungumza na
wananchi na wanachama wa ADC mara baada ya kuchukuwa fomu ya Urasi huko katika
ofisi za chama hicho Wawi kibegi kisiwani Pemba.
Na Abdi Suleiman na Abdi
Shamnah,PEMBA.
ALIYEKUWA mwanachama wa chama cha
CUF na mbunge wa jimbo la wawi kisiwani Pemba, ambaye kwa sasa amehamia chama
cha ADC Hamad Rashid Mohamed, Leo amechukuwa fomu ya kugombea urais wa Zanzibar
kupitia chake hicho.
Fomu
hiyo aliyokabidhiwa leo na kamishna wa ADC Kanda ya Pemba, Said Seif huko
katika ofisi za chama hicho Wawi kibegi Wilaya ya Chake Chake Pemba.
Akitoa
nasaha zake Mara baada ya kuchukuwa fomu hiyo, Mgombea huyo Hamad Rashid,
alisema hatua hiyo ya kuchukuwa kweke fomu inalenga kuleta mabadiliko makubwa
ya kisiasa Zanzibar.
Alisema
kuwepo kwa chama hicho ni kuondosha dhana iliyojengeka miongoni mwa wananchi wa
Zanzibar, pamoja na viongozi wa vyama vya upinzani kwamba vyama vya CCM
na CUF ndio vyama vyenye uhalali wa kuongoza nchi.
Alisema
hatua ya wananchi wa Pemba kujitokeza na kumpokea kwa wingi ni thibitisho tosha
kwa wananchi kuwa wamejenga imani nayeye na wamekubali mabadiliko ili
kuelekeza nchi hiyo katika maendeleo ya kweli.
"Leo
ni siku ya historia katika chama cha ADC tokea miaka tatu kuwepo kwao, kimeweza
kutoa mabadiliko makubwa kufikia kupatikana mgombe wa urais wa Zanzibar"
alisema Hamad Rashid.
Aidha
aliwapongeza wananchi na viongozi wa ADC kwa ujasiri wao mkubwa wa kuanzisha
chama hicho, huku baadhi ya watu na viongozi wa upinzani wakiona hatua hiyo
kwamba ni dhambi.
Aliwataka
wananchi kisiwani Pemba kuendeleza imani na chama hicho na kuondokana na dhana
kwamba CUF ndio chama pekee chenye uwezo wa kuwapelekea maendeleo, huku
akibeza kisiwa hicho kubaki nyuma kimaendeleo.
Mgombea
huyo wa ADC anatarajiwa kurudisha fomu hiyo Julai 28 mwaka huu, Kwa katibu mkuu
wa chama hicho Unguja, kabla ya kuchukuwa fomu ya Serikali ya kugombea urais wa
Zanzibar.
Mapema
kamishna wa ADC kanda ya Pemba Said Seif alimshukuru mgombea huyo kwa ujasiri
na uamuzi wake wa kujitokeza kuchukuwa fomu ya kugombea urais wa Zanzibar
kupitia ADC.
"Hiki
ni kitendo cha kihistoria kwa mlezi wetu kujitokeza kuchukuwa fomu, sisi
wananchi na wanachama wa ADC tuko pamoja na yeye"alisema.
Alisema
mgombea huyo ni kiongozi shupavu na aliyekomaa kisiasa, huku wananchi wakiwa na
matumaini makubwa kutoka kwake katika kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye
nafasi ya urais wa Zanzibar.
No comments:
Post a Comment