Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Mwinyi Ametowa Mkono wa Pole kwa Familia ya Marehemu Sheikh.Jabir Haidar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsalimia na kutowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu Sheikh. Jabir bin Haidar bin Jabir Al-Farsy, alipofika nyumbani kwa Kaka wa marehemu mtaa wa Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja leo 6-6-2025 kwa ajili ya kutowa mkono wa pole kwa familia hiyo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kutowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu Sheikh.Jabir bin Haidar bin Jabir Al-Farsy, alipofika nyumbani kwa kaka wa Marehemu mtaa wa Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja leo 6-6-2025 na (kushoto kwa Rais) Kaka wa Marehemu Kassim Haidar na (kulia kwa Rais) Watoto wa Marehemu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Familia ya Marehemu Sheikh.Jabir bin Haidar bin Jabir Al-Farsy, kuitikia dua ya kumuombea marehemu,baada ya kutowa mkono wa pole kwa familia nyumbani kwa Kaka wa Marehemu mtaa wa Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar leo 6-6-2025
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.