Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Shaib Ibrahim Muhamed amesema wataendelea kuwasaidia, kuwaendeleza na kuwawezesha Vijana wa Zanzibar ili kuweza kujikwamua kiuchumi .
Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Kariakoo wakati wa Kikào cha robo mwaka cha Uratibu wa shughuli za Maendeleo ya Vijana Zanzibar.
Amesema jukumu la Idara hiyo ni kuratibu na kusimamia Vijana kupitia Baraza la Vijana kwa kuwapa muongozo wa kitaifa na kuwapatia taaluma ya kuwajengea uwezo ili kuhakikisha shughuli mbali mbali za maendeleo ya Vijana zinafanyika ipasavyo.
Aidha amewataka Vijana hao kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwa Amani na utulivu ili kuendeleza Uzalendo wa nchi yao.
Nae Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Ali Haji Hassan amesemà Serikali imeanzisha Mabaraza ya Vijana Kwa lengo la kuimarisha mashirikiano ya Vijana na Wadau Mbali mbali katika ngazi ya Sheria na Wilaya ili kufikia malengo ya kuwainua Vijana .
Kwa Upande wa Muakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu ( UNFPA) na Masuala afya ya Uzazi . Amina Kheir amewataka Vijana kutengeneza programu endelevu Kwa kujiendeleza kiuchumi kutokana na Wafadhili kuanza kupungua duniani .
Amesema kutokana kupungua kwa Wafadhili wa Wakala wa Kimarekani wa Msaada wa Maendeleo ya Kimataifa (USAID) hivyo ni vyema Vijana kushirikiana kwa pamoja katika Taasisi mbali mbali kwa kutengeneza Programu ambayo itawasaidia kupata kipato katika Kazi za staha kwa wote.
Akitoa Muhtasari wa taarifa za utekelezaji wa mwaka 2024 Hadi 2025 Mratibu wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar Ndugu Salma Kombo Mohamed amesemà jumla ya Vijana laki 325 Wamapatiwa mafunzo ya Ujasiriamali na Uwezeshaji, Stadi za Maisha , Ushiriki na Ushirikishwaji , Afya ya Uzazi , Uongozi na Uzalendo, Mazingira ya Tabia ya nchi pamoja na Teknolojia na Mawasiliano .
Amesemà katika kitini Cha Stadi ya Maisha wameweza kutoa mafunzo Kwa Vijana 21 ambao walikuwa nje ya skuli na kutoa mafunzo ya afya ya Uzazi Kwa Vijana 73,240 Kwa Unguja na Pemba .
Kwa Upande wa Afisa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi Juma Rashid Ali akiwasilisha mada juu ya mambo muhimu kwa Vijana kuelekea Uchaguzi mkuu amesisitiza kutunza heshima nidhamu na maadili Kwa kuachana na mihemko wakati wa Kampeni ,Uchaguzi na kipindi cha matokeo ili kutunza Amani na utulivu wa nchi .
Kwa Upande wa Vijana hao wameiomba Idara ya Vijana kuwapatia mafunzo ya Fedha katika vikundi mbali mbali ili kuweza kuwasaidia kukidhi sifa za kupatiwa mikopo na kumudu kufanya marejesho.
Baadhi ya Vijana walioshiriki Kikao cha robo mwaka cha Uratibu wa shughuli za Maendeleo ya Vijana Zanzibar.wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Shaib Ibrahim Muhamed (hayupo pichani) katika Ukumbi wa Kariakoo,Wilaya ya Mjini .
Afisa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi Juma Rashid Ali akiwasilisha mada juu ya mambo muhimu kwa Vijana kuelekea Uchaguzi mkuu Kwa makundi ya Vijana katika Ukumbi wa Kariakoo,Wilaya ya Mjini .
Imetolewa na Kitengo Cha Habari.
WHVUM.
No comments:
Post a Comment