Habari za Punde

Whatsapp kufungiwa Uingereza?


Mtandao maarufu wa social media whatsapp huenda ukafungiwa nchini Uingereza ikiwa sheria mpya inayojulikana kama ‘Snoopers’ Charter itapitishwa na Bunge la nchi hiyo linaloongozwa na chama cha Conservative.

Sheria hii imo kwenye muswada wa Sheria, Communications Data Bill ambao uliletwa bungeni mwaka jana lakini upande wa Liberal Democrats ambao ulikuwa serikalini wakati huo iliukataa.

Kwa kuwa Conservative walishinda uchaguzi na kuwa na uwezo wa kupitisha muswada wowote kwa sasa kuna uwezekano mkubwa muswada huu utaweza kupitishwa na kuwa sheria.

Sheria hii inazitaka kampuni zinazomiliki mitandao kutunza na kuhifadhi mazungumzo ya wateja wao kwa muda wa miezi 12 baada ya kutokea.


Kwa kuwa whatsapp, snapchat na iMessage hutuma ujumbe kwa njia ya encyprted ambayo huwa vigumu kwa mtu mwengine kuweza kujua kilichomo kwenye ujumbe, Serikali imesema itaweza kutumiwa na magaidi kuweza kuwasiliana na kutumia na ujumbe bila ya kugundulika. 

Hivyo watazitaka kampuni hizi ima zibadilishe utaratibu wao vyenginevyo zitaweza kufungiwa kwani tishio la ugaidi ni kwa maslahi ya wananchi wengi ambao wataweza kuathirika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.