Habari za Punde

Dk Shein atuma salamu za rambirambi Mfalme wa Dubai kufuatia kifo cha mwanawe

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
 Zanzibar                                                           3.8.2015
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za rambirambi Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE) na Mfalme wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al-Maktoum kufuatia kifo cha mwanawe Sheikh Rashid bin Mohammed Al- Maktoum.

Katika salamu hizo za rambirambi, Dk. Shein alisema kuwa kwa niaba yake, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na wananchi wa Zanzibar wanatoa mkono wa pole kufuatia kifo hicho.

Aidha, salamu hizo za rambirambi zilimuombea Dua kwa MwenyeziMungu Kiongozi huyo wa UAE pamoja na Wanafamilia wa Al-Maktoum na kuwaomba kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo.

Dk. Shein amemuomba Mwenyezi Mungu kuilaza roho ya marehemu mahala pema peponi, Amin.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.