Habari za Punde

Warsha ya kuhamasisha utumiaji wa vyakula vya mboga mboga na matunda


WANAFUNZI waskuli mbali mbali kisiwani Pemba, wakipitia kwa makini maelezo yanayoelezea jinsi ya kutumia vyakula vya matunda na mboga mboga, wakati wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Jumuiya ya wanafunzi wa Tanzania waliosoma Japani(JATA).(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KAIMU Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Tanzania waliosoma Japani (JATA) Mbarouk Talib, akizungumza na wanafunzi wa skuli mbali mbali za Sekondari kisiwani Pemba, huko katika ukumbi wa Fidel Castro.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 Mkurugenzi Mkaazi wa JICA Tanzania Mhe: Toshio Nagase, akizungumza na wanafunzi wa skuli mbali mbali za sekondari kisiwani Pemba, huko katika skuli ya Fidel Castro juu ya kuhamasisha utumiaji wa vyakula vya mboga mboga na matunda .(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KATIBU Tawala Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Ahmed Khalid akifungua warsha ya siku moja kwa wanafunzi wa skuli za sekondari kisiwani Pemba, huko katika skuli ya Fidel Castro juu ya uhamasishaji wa utumiaji wa vyakula vya mboga mboga na matunda.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KATIBU Mtendaji wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Tanzania waliosoma Japani (JATA) Selina Lyimo, akitoa neon la shukurani kwa mgeni rasmi baada ya kufungua warsha hiyo ya siku moja kwa wanafunzi wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 MKUU wa Idara ya Kinga Wizara ya Afya Pemba dk. Shaibu Itibar, akiwasilisha mada ya Virutibisho katika warsha ya siku moja, iliyowashirikisha wanafunzi mbali mbali kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MRATIBI wa kitengo cha kilimo cha Umwagiliaji kwa kutumia matonye ya maji, kutoka JICA Tanzania Hideyuki Morri, akiwasilisha mada ya umwagiliaji kwa wanafunzi wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WANAFUNZI wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba wakiuliza maswali, juu ya uendelezaji wa kilimo cha mboga mboga na matunda, kupitia mradi wa Umwagiliaji maji uliobuniwa na wanachama wa JATA Tanzania.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 MMOJA wa wanachama wa JATA Tanzania akiwafahamisha wanafunzi namna ya kilimo cha umwagiliaji maji kwa kutumia matonye inavyofanya kazi.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.