Habari za Punde

Mkutano wa kampeni za CCM uwanja wa Misuka jimbo la Donge

 Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar pia Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM Taifa (NEC) Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wakati alipowasili katika uwanja wa Misuka katika mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM katika jimbo la Donge mkoa wa Kaskazini Unguja.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum Haji Omar Kheir akiwasalimia wananchi na wanachama wa Jimbo la Donge wilaya ya Kaskazini B Unguja wakati wa mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo uwanja wa Misuka Mahonda.
 Baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM waliojitokeza katika mkutano wa kampeni za CCM Jimbo la Donge katika uwanja wa Misuka kijiji cha Mahonda wilaya ya Kaskazini B mkoawa Kaskazini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa  msera za Chama hicho leo.
 Aliyekuwa Balozi  Umoja wa Afrika nchini Marekani Mama Amina Salum Ali akiwasalimia Maelfu ya Wananchi na Wanachama wa CCM Jimbo la Donge Wilaya ya Kaskazini B Unguja katika  mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo uwanja wa Misuka Mahonda,ambao mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.
 Baadhi ya Viongozi na wagombea nafasi za Ubunge,Uwakilishi na Udiwani wakiwa katika jukwaa wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akiwanadi kwa Wananchi wakati wa mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo uwanja wa Misuka Mahonda Jimbo la Donge Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwasalimia  maelfu ya wananchi na wanaCCM wakati alipozungumza nao katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM  uliofanyika leo katika uwanja wa Misuka Mahonda,Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja  Jimbo la Donge, katika mwendelezo wa Mikutano mbalimbali  ya hadhara katika Mikoa ya Unguja na Pemba.

 Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakishangilia sera zilizotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein leo katika mkutano wa hadhara wa kampeni  za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo katika Jimbo la Donge Mkoa wa  Kaskazini Unguja.
  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Waziri wa Ardhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban akitoa ufafanuzi kuhusu suala la Mafuta kwa wananchi wa Jimbo la Donge katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi zilizofanyika leo katika uwanja wa Misuka Mahonda Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.