Habari za Punde

Halotel kuandaa matamasha ya Christmas katika mikoa mitano nchini



Kampuni ya simu za mikononi ya Halotel inaandaa matamasha ya Christmass katika mikoa mitano nchini yenye lengo la kuwapa burudani watuamiaji wa mtandao huo pamoja na wale watakaohitaji kujiunga na mtandao huo.

Matamasha hayo ambayo yatafanyika wilaya za Tukuyu, Ruangwa, Moshi Vijijini, Chato pamoja na Mpwapwa, yatajumuisha wasanii wa bongo fleva pamoja na burudani nyingine kutoka kwa wasanii wa maeneo hayo.

Tamasha la Halo Christmass wilayani Tukuyu litafanyika katika uwanja wa Tandale na burudani itatolewa na wasanii Tundaman na Makomando.

Kwa upande wa Ruangwa, tamasha hilo litafanyika katika viwanja vya shule ya msingi Likangala, na kutumbuizwa na wasanii Amini pamoja na Matonya, wakati Mpwapwa tamasha litafanyika katika viwanja vya Mgambo likitumbuizwa na wasanii Madee na Malaika.

Tamasha hilo pia litafanyika wilayani Chato katika viwanja vya Stand ya Zamani huku burudani ikitolewa na msanii Shetta na Baraka Da Prince.

Wakazi wa Moshi vijijini pia watafurahia tamasha la Christmass kwa burudani Shilole na Msami zitakazofanyika katika viwanja vya Kae.


Akizungumzia matamasha hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Halotel bwana Nguyen Thanh Quang, amesema matamasha hayo ya Halotel yanalenga kuwaleta watumiaji wa Halotel pamoja na kuwapa burudani ya kufunga mwaka.

‘Hii ni zawadi kwa watumiaji wa mtandao wetu na wateja wapya wanaotaka kujiunga na familia yetu ya Halotel, na ndio maana tunawafata katika maeneo yao yalipo’ alisema Quang.

Matamasha hayo yatafanyika kuanzia saa sita mchana hadi saa kumi na mbili jioni, na kiingilio itakuwa ni laini ya mtandao wa Halotel kwa wateja wapya huku wale wenye laini za Halotel tayari wakiingia bure.

Quang pia amewaahidi wateja wa Halotel kuwa mtandao wake unatarajia kuleta mabadiliko katika sekta ya mawasiliano nchini kwa kuwapa wateja wake zaidi ya huduma za simu.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.