Sehemu ya wizi wa maji kutoka katika mtandao wa DAWASCO unavyoonekana kufanywa katika kiwanda cha kutengenezea Betri cha Bahari Chemicals Ltd.
Ikiwa
siku chache tu zimepita baada ya shirika la Majisafi
na Majitaka Dar es salaam
(Dawasco) kubaini wizi mkubwa wa Maji kutumika katika shamba la mboga mboga na
matunda katika chuo cha Islamic kilichopo Boko ununio jijini Dar es salaam.
Dawasco imebaini wizi mwingine wa Maji katika kiwanda cha kutengeneza Maji ya
betri cha Bahari Chemicals Ltd kilichopo kurasini wilaya ya Temeke jijini Dar
es salaam.
Akizungumzia
tukio hilo meneja wa Dawasco Temeke, Bw.
Deogratius Rwegasira, amethibitisha
kutokea kwa wizi huo
ambapo kiwanda hicho kilikuwa kimejiunganishia Maji bila
kibali cha Dawasco na kwamba hawakuwa na mita wala
akaunti namba inayoonyesha
kiasi cha Maji kinachopita
katika system ya Maji iliyopo, na baada ya kufanya
mawasiliano na Mkurugenzi wa kiwanda hicho
Bw.Devendra Singh Parmar amekiri
kutumia Maji hayo
kinyume na taratibu .
“Baada
ya kufanya uchunguzi tumebaini kuwa kiwanda hiki
kimekuwa kikituibia Maji yetu
kwa muda mrefu, mmiliki wa
kiwanda amekubali kosa,lakini akisema kwamba wenyewe
ni wageni hapa hawana zaidi ya mwaka mmoja tangu
waanze kazi.hivyo hawakujua
taratibu za kufuata”. Alisema
Bw. Rwegasira.
Aidha
meneja wa kiwanda hicho, Bw. Abdul Gulam, amekiri
kuihujumu Dawasco kwa kuiibia
Maji, lakini amesema kuwa
wao ni wapangaji tu wamepanga katika eneo hilo na
wana
muda wa miezi saba tangu wahamie kiwandani hapo,
walikuta wizi huo wa Maji
ukifanyika katika kiwanda hicho
na
hawakujua taratibu husika za kufuata ili wapate huduma
ya Maji kihalali.
“Sisi
tumekubali kuwa tulikuwa tunatumia Maji ya
DAWASCO bila kuyalipia, lakini sio
sisi ambao
tuliounganisha bomba hili, wapangaji waliopita
walijiunganishia Maji
haya hivyo tunaomba tulimalize hili, ili
tuanze kuwa wateja wenu rasmi” alisema
Bw.Gulam.
Aidha
bwn Gulam ameainisha kuwa wao kama wamiliki wa
kiwanda wamekubali kulipa faini
iliyotolewa na DAWASCO
ya Shiling million 3.5 ili warudishiwe huduma kama
wateja
wengine na waweze kuendelea na biashara.
Vitendo
vya uhujumu wa Miundombinu ya Maji hususani
wizi wa Maji unaendelea kuwa
changamoto kwa
DAWASCO licha ya kampeni na elimu inayotolewa kila siku
juu ya
uhalali na utaratibu wa kuungiwa huduma ya Maji
inayotolewa na DAWASCO.
Imeandaliwa na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii.
|
No comments:
Post a Comment