Habari za Punde

Mafunzo ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria yafanyika Pemba

 MRATIBU wa mafunzo ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria Safia Saleh Sultan akielezea mafunzo hayo kwa waratib wa shehia za Mkoa wa kaskazini Pemba, mafunzo yaliofanyika ukumbi wa mikutano wa Kituo cha Huduma za Sheria Chakechake, kulia ni Mratibu wa Kituo Fatma Khamis Hemed na katikati ni Afisa Mdhamini wizara ya wanawake na watoto Pemba, Mauwa Makame Rajab, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WARATIBU wa shehia za mkoa wa kaskazini Pemba, wakiwa makini kusikiliza mada zinazowasilishwa kwenye mafunzo ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria, mafunzo hayo yameandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria na kufanyika afisini kwao mjini Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 AFISA Mdhamini wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii Vijana Wanawake na watoto Pemba, Mauwa Makame Rajab akifungua mafunzo ya siku moja ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria, mafunzo yaliofanyika Kituo cha Huduma za Sheria Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MTOA mada ya haki za binadamu Safia Saleh Sultan kutoka Kituo cha Sheria, akiwasilisha mada hiyo kwenye mafunzo ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria, mafunzo yaliofanyika kituoni hapo mjini Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MTOA mada ya dhana ya wasaidizi wa sheria majimboni Fatma Khamis Hemed, kutoka Kituo cha Sheria, akiwasilisha mada hiyo kwenye mafunzo ya kutambulisha kazi za wasaidizi wa sheria, mafunzo yaliofanyika kituoni hapo mjini Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.