Habari za Punde

Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilipotembelea Miradi jijini Dar es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira, Mheshimiwa January Makamba akinyoosha mkono kuonesha Mradi wa Kingo za Fukwe  unaosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi wakati Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilipotembelea  Mradi huo jijini Dar es Salaam leo.



 Sehemu ya Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Bihashara na Mazingira wakifatilia kwa makini Taarifa ya Mradi wa Jengo la Baraza la Taifa la Hifadhi na  Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza hilo, Mhandisi Bonaventure Baya (hayupo pichani).
 Sehemu ya Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira wakitembelea eneo la Mradi wa Kingo za Fukwe jijini Dar es Salaam, mradi huo umeanzishwa  kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na  unasimamiwa na Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira, Mheshimiwa January Makamba akiwa na Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira wakati wa walipotembelea Mradi wa Jengo la Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), anayetoa maelezo mbele yao ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza hilo, Mhandisi Bonaventure Baya.

Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.