Aleyekuwa Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar Balozi Ali Abdalla Al-Rashid aliyefariki Dunia juzi kwa usiku katika Hospitali ya Global kwa ugonjwa wa shindikizo la damu .
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na viongozi wa serikali wakiuanga mwili wa Balozi mdogo wa Oman zanzibar bwa Ali Abdalla al-Rashid aliyefariki jana kwa ugonjwa shindikizo la damu katika hospital ya global zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kusafirisha mwili wa Balozi mdogo wa Oman nchini Zanzibar katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani karume Zanzibar
Na Mwandishi Wetu
Balozi mdogo wa Zanzibar aliyepo Zanzibar, Mhe. Ali Abdallah Al-Rashid amefariki dunia juzi usiku katika hospitali ya Global baada ya kukabiliwa na shindikizo la damu.
Kufuatia kifo hicho, viongozi mbalimbali wa vyama na serikali na wananchi walishiriki kuuaga mwili wa marehemu ambapo Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliongoza msiba huo.
Viongozi hao pia walishiriki kuusafirisha mwili wa marehemu kuelekea Oman kwa ajili ya mazishi katika Uwanja wa Ndege wa Zanzibar kwa Shirika la Ndege la Oman majira ya saa 8:00 mchana hapo jana.
Akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif, alisema Oman na Zanzibar zina uhusiano mkubwa katika kuimarisha mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na masuala ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni
.
.
Aidha, aliongeza kuwa msiba huo ni mkubwa siyo kwa Oman pekee lakini hata kwa Zanzibar kwani umeacha pengo kubwa kwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Balozi Seif pia alitoa pole kwa wananchi wa Oman na Zanzibar kwa msiba huo.
Wakati huo huo, Mkurugenzi Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Zanzibar, Balozi Silima Ali Kombo Haji, alielezea kusikitishwa na kifo cha Balozi Al-Rashid ambaye alikuwa ni mtu mwenye hekima na busara.
No comments:
Post a Comment