Habari za Punde

Wajumbe BLW Wakiwasili Mjengo kuhudhuria Mkutano wa Baraza la Wawakilishi kusikiliza Hutuba ya Bajeti Mwaka 2016/2017

Jengo la Baraza la Wawakilishi Zanzibar. 
 Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Mhe.Juma Ali Khatib akiwa na Kiongozi wa Chama cha AD TADEA Mhe Mchenga wakiwasili katika viwanja vya Baraza kuhudhuria Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wawakilishi ulioanza leo kwa hutuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, akiwasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi kuhudhuria Mkutano wa Tisa wa Baraza kwa kusomwa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mwakilishi wa Jimbo la Chaani Zanzibar Mhe Nadir Abdullatif akiwasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi.
Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakiwasili katika viwanja vya Baraza kuhudhuria Mkutano wa Tisa wa Baraza. 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.