Habari za Punde

Waziri wa biashara, viwanda na masoko atembelea maghala ya kuhifadhia vyakula kuelekea mwezi mtukufu wa Ramadhan

 MENEJA Mkuu wa kampuni ya Evergreen Abdulghafar Ismail Mohammed  akimfahamisha Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko  Amina Salum Ali juu ya hali ya chakula nchini alipotembelea katika ghala lake Saateni mjini Zanzibar.
 BAADHI  ya vyakula  vilivyohifadhiwa katika ghala la kampuni ya Evergreen Saateni mjini Zanzibar.

 WAZIRI Amina Salum Ali akiangalia vyakula vilivyohifadhiwa katika ghala la kampuni ya Evergreen lililopo Saateni mjini Zanzibar.

 WAZIRI wa Biashara, Viwanda na Masoko Amina Salum Ali akisaini kitabu cha wageni alipotembelea kiwanda cha Zanzibar Milling Corporation kilichoko Mtoni nje kidogo  ya mji wa Zanzibar.


 MENEJA Mkuu wa kiwanda cha Zanzibar Miling Corporation  Khalid Ali Yussuf, akimpa maelezo Waziri  Amina Salum Ali juu ya uzalishaji wa chakula alipotembelea ofisini kwake  Mtoni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
 WAZIRI wa Biashara, Viwanda na Masoko Amina Salum Ali akiwa katika maeneo ya kiwanda  cha Zanzibar Miling Corporation Mtoni alipofanya ziara maalum kwa ajili ya kuangalia hali ya chakula nchini wakati huu wa kuelekea mwezi mtukufu wa Ramadhan. 
 WAZIRI wa Biashara, Viwanda na Masoko Amina Salum Ali akioneshwa  ngano na Meneja Mkuu wa kiwanda cha Zanzibar Milling kilichoko Mtoni Zanzibar Khalid Ali Yussuf, katika sehemu ya usagishaji alipotembelea kiwanda hicho.
MENEJA Mkuu wa kampuni ya Bopar Enterprises Said Nassir Said, akizungumza na Waziri  Amina Salum Ali wakati Waziri huyo alipomtembelea ofisini kwake Mombasa mjini Zanzibar.
PICHA ZOTE NA ABDALLA OMAR – HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.