Naibu
Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano
na Mazingira Mh.Luhaga Mpina akiongea na waandishi wa habari mara baada ya
kupiga faini viwanda vitatu ambavyo vimetuhumiwa kuchafua mazingira wilaya ya
temeke mtaa wa serengeti.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na
Mazingira Mh,Luhaga Mpina akipata maelezo kutoka kwa uongozi wa kiwanda cha bia
serengeti alipofanya ziara ya kukagua Mazingira katika eneo hilo la viwanda
linalotuhumiwa kuchafua mazingira.
Naibu
waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano
na Mazingira Mh, Luhaga Mpina akipata maelezo kutoka kwa mbunge wa temeke
mh,Abdallah Mtolea kuhusu uchafuzi wa mazingira wilaya ya temeke mapema hii
leo
Na Evelyn Mkokoin. Dar es Salaam.
Kampuni ya usafirishaji ya Kanji Lalji iliyopo mtaa wa
Serengeti
wilayani Temeke jijini Dar es Salaam imetozwa faini ya shilingi
milioni ishirini na laki tano, na kutakiwa kulipa faini hiyo ndani ya
siku
saba, kwa kosa la kutiririsha maji yenye sumu katika mitaro
ya maji ya mvua
inayoelekea kwenye makazi ya watu na mazingira na hivyo kuhatarisha maisha na
afya za viumbe hai.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira
ametoa kauli hiyo leo kupitia Baraza la Taifa na Hifadhi ya
Mazingira NEMC
katika ziara yake ya kukagua viwanda na usafi
wa mazingira jijini dar es salaam.
Ziara hiyo ya Naibu waziri Mpina, iliyopelekea naibu waziri
huyo
kuinuka Ofisini na kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika baadhi
ya viwanda
hivyo, imetokana na malalamiko ya baadhi ya wanachi katika maeneo husika
hususan wenye viwanda.
Naibu waziri mpina amesema kuwa kutozwa faini ni hatua ya
pili
kwa baadhi ya viwanda baada ya kupewa onyo na maelekezo na
NEMC na
manispaa, na aliongeza kuwa kwa kutokutii taasisi za
serikali baada ya adhabu
hii hatua itakayofuata ni ya kuvifungia
viwanda hivyo.
Kwa upande mwingine Mhe. Mpina amekipongeza kiwanda cha
Serengeti breweries kwa kutii kauli ya serikali kwa kulipa faini
iliyotozwa
awali ya kiasi cha shilingi milioni kumi na sita kwa
kosa la uchafuzi wa
mazingira na kuwashukuru wakazi wanaozunguka kiwanda cha SBL pamoja na Mbunge wa
TEMEME (CUF) Mhe.Abdallah Mtolea kwa kutoa taarifa za uchafuzi wa mazingira na
kukipa kiwanda hicho siku 45 kufanya marekebisho madogo madogo ya kimazingira
kiwandani hapo.
Aidha, Adhabu nyingine ya uharibifu na uchafuzi wa mazingira
imetolewa kwa wamiliki wa eneo la kampuni ya CI group, ambao
ni Prime Liberty
Limited ya kutakiwa kulipa faini ya shilingi
milioni 15 kwa muda wa siku saba,
na kufanya jumla ya faini za
uchafuzi wa mazingira zilizotozwa kwa siku ya leo
kuwa shilingi
milioni 39 na laki tano.
No comments:
Post a Comment