Habari za Punde

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe azikwa leo

 Mwili wa Aliekuwa Rais wa Serikali ya Zanzibar awamu ya Pili  marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam ukiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Zanzibar.
 Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabi katikati akiupokea mwili wa aliekuwa Rais wa Serikali ya  ZanzibarAwamu ya pili  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi kwa kuuombea dua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar
 Nyuso za Huzuni zatawala nyumbani kwa marehemu Migombani zanzibar baada ya kuwasili kwa mwili wa Mzee wao aliekuwa Rais wa Serikali ya  Zanzibar Awamu ya Pili  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam.
 Rais wa Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein katikati akiomba dua pamoja na viongozi mbalimbali katika jeneza lililowekwa Mwili wa aliekuwa Rais  wa Seriali ya  Zanzibar Awamu ya Pili Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam. Nyumbani kwake Migombani Zanzibar.

 Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akimpa mkono wa Pole Kapteni Abdalla Yussuf Jumbe(Ami wa marehemu)baada ya kuwasili nyumbani kwake migombani mjini Zanzibar.

 Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan wamwanzo kushoto akiomba dua katika Jeneza lililowekwa Mwili wa aliekuwa Rais wa Serikali ya  Zanzibar Awamu ya pili  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam. Nyumbani kwake Migombani Zanzibar.
 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akiomba dua katika Jeneza lililowekwa Mwili wa aliekuwa Rais  wa Serikali ya  Zanzibar Awamu ya pili Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam. Nyumbani kwake Migombani Zanzibar.
 Umma wa watu mbalimbali waliohudhuria katika maziko ya aliekuwa Rais  wa  Serikali ya Zanzibar Awamu ya pili Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam. hapo Nyumbani kwake Migombani Zanzibar
  Umma wa watu mbalimbali waliohudhuria katika maziko ya aliekuwa Rais  wa  Serikali ya Zanzibar Awamu ya pili Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliefariki jana Dare es salaam. hapo Nyumbani kwake Migombani Zanzibar
 Kiongozi wa Familia ya marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliekuwa Rais  wa Serikali ya  Zanzibar awamu ya pili Mustafa Abod Jumbe akibeba jeneza liliokuwa na mwili wa Marehemu baba yake kuingiza katika msikiti wa Mushawwara Rahaleo kwa ajili ya kusaliwa.
 Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohd Shein akimimina mchanga katika kaburi la aliekuwa Rais  wa Serikali ya Zanzibar awamu ya pili Mzee Abou Jumbe Mwinyi alifariki jana Dare es salaam.

Marehemu amezikwa nyumbani kwake Migombani Zanzibar.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi akimimina mchanga katika kaburi la aliekuwa Rais  wa Serikali ya Zanzibar awamu ya pili Mzee Abou Jumbe Mwinyi alifariki jana Dare es salaam.marehemu amezikwa nyumbani kwake Migombani Zanzibar.

PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.