Habari za Punde

Wananchi kijiji cha Ndagaa walalamika wizi wa mazao

Na Fatma Makame/Maida Hamza MCC          
                                           
Wananchi  wa kijiji  cha Ndagaa Wilaya Kati Unguja, wamelalamikia vitendo vya wizi wa mazao yao vinavyofanywa na baadhi ya vijana wasiopenda kufanyakazi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkaazi wa kijiji hicho bi. safia seif amesema vijana hao wasiopenda  kufanyakazi wanarudisha nyuma maendeleo yao  na kushindwa  kufikia malengo waliyojiwekea.

Amesema vijana hao wamekuwa wakifanya vitendo vya wizi wakati wa usiku mkubwa na imekuwa vigumu kuwakamata licha ya juhudi za kuwavizia  zinazofanywa na wakulima.

Ameongeza kuwa vijana hao wanapoingia kwenye mashamba yao hawachagui mazao na hata mazao machanga huwa wanayachuma.

Amezitaka mamlaka husika zikiwemo  taasisi za kilimo na masoko yanayotumika kuuzia mazao kuangalia bidhaa hizo na zile ambazo hazijafikia kiwango cha kuvunwa kuzuiliwa kuuzwa katika masoko hayo ili kuepuka wimbi la kuuza mazao machanga.

Nae Bwana Salum Seif Hamad amesema tabia ya kuibiwa mazao yao  imekuwa ni ya muda mrefu  sasa na bado hawajapata  dawa  ya tatizo hilo.

Ameiomba serikali kutoa adhabu kali kwa vijana wanaojishughulisha na wizi wa mazao ili kuwa fundisho kwa vijana wenye tabia hiyo.

 Ametoa wito kwa vijana kujishughulisha na kazi yeyote  ya  halali  inayoweza kuwapatia  tija bila kutegemea ajira kutoka serikalini. 

Wachimbaji wa kifusi kwa ajili ya kusaga kokoto  wa kiwanda cha Mwera Pongwe wameiomba serikali kuboresha miundo mbinu ya barabara inayoelekea katika kiwanda hicho ili  kuinua kipato chao na taifa kwa jumla .

Akizungumza na mwandishi wa habari Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Rashid Khatibu Hamad amesema barabara hiyo inasababisha usumbufu mkubwa kwa wateja wao na baadhi ya gari hushindwa kufika.

Amesema kiwanda hicho kimekuwa msaada mkubwa kwa  vijana wengi kupata ajira na iwapo barabara hiyo itaboreshwa kiwanda kinaweza kutoa mchango mkubwa zaidi kwa taifa .

Ameongeza kuwa tatizo jengine linalokikabili kiwanda hicho, baadhi ya wateja wanakosa   uaminifu, baada ya kukopeshwa hushindwa  kulipa  kwa wakati jambo  linalorudisha  nyuma maendeleo ya kiwanda hicho

Wanunuzi wa kokoto na kifusi wa kiwanda hicho  wameiomba serikali kuwapunguzia ushuru wamiliki wa kiwanda hicho kwa vile  wamekuwa wakinunua bidhaa hizo kwa bei kubwa kutokana na kiwanda kulipa ushuru mkubwa.

Aidha wamewataka vijana kujishughulisha na kazi  za ujasiriamali  na kuacha tabia ya kukaa katika vikundi  viovu bila kufanya kazi.
                                                      

IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.