Na.Rajab.Mkasaba. Pemba.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein ametoa pongezi za dhati kwa wanawake wote wa Unguja na Pemba kwa kujitokeza katika kuwania nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi mkuu uliopita, hapa Zanzibar na Tanzania nzima kuanzia nafasi ya Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein ametoa pongezi za dhati kwa wanawake wote wa Unguja na Pemba kwa kujitokeza katika kuwania nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi mkuu uliopita, hapa Zanzibar na Tanzania nzima kuanzia nafasi ya Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.
Mama Mwanamwema Shein aliyasema hayo huko
katika ukumbi wa Skuli mpya ya Sekondari ya Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba
katika mkutano kati yake na Viongozi wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) wa
Wilaya ya Mkoani, mkutano wenye lengo la kusalimiana, kupongezana na
kubadilishana mawazo.
Katika maelezo yake Mama Shein, alitoa
pongezi maalum kwa wanawake wote waliojitokeza kuwania nafasi hizo na wakaweza
kuibuka kuwa washindi katika nafasi ya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.
Alisema kuwa ushindi uliopatikana ni
muhimu sana kwa maendeleo ya wanawake na wananchi wa Zanzibar na Tanzania nzima
kwa jumla kwani ushindi huo umeongeza ushiriki katika nafasi za uongozi wa juu
na kuwaweka katika nafasi nzuri kwenye suala zima la kufanya maamuzi ya nchi
yao.
Mama Shein alisema kuwa ni faraja kubwa
kwa wanawake kuona kwamba Serikali zote mbili zilizopo madarakani hivi sasa
zina hamasisha na kuunga mkono ushitriki wa wanawake katika nafasi za uongozi
kwa kuwapa nafasi mbali mbali za uongozi.
Aidha, Mama Shein alitoa shukurani kwa
uongozi wa Serikaloi ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dk. Ali
Mohamed Shein, kwa kutoa nafasi nyingi za uongozi kwa vijana na wanawake na
kutoa wito kwa akina mama wenzake kuendelea kuwa watendaji wazuri, wenye bidii
na uadilifu.
Katika mkutano huo jumla ya wanachama
wapya 30 waliojiunga na Jumuiya ya UWT walikabidhiwa kadi za Jumuiya hiyo na
Mama Mwanamwema Shein.
Nae Mke wa Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar, Mama Asha Balozi alitumia fursa hiyo kuwapongeza na kuwashukuru
wanachama na viongozi wa Jumuiya hiyo huku akiwasisitiza kuendeleza amani na
utulivu hapa nchini.
Mjane wa Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,
Mama Fatma Karume nae alitumia fursa hiyo kutoa historia ya wanawake kabla na
baada ya Mapinduzi na kuwasisitiza wanachama na viongozi wa Jumuiya hiyo
kutumia muda wao kusoma historia ya Zanzibar.
Aidha, alisema kuwa mbali ya wao kuijua
na kuisoma historia ya Zanzibar pia, alieleza haja ya kuwafahamisha na
kuwafundisha vijana na watoto wao historia ya Zanzibar kwa kujua walipotoka,
walipo na wanakokwenda.
Nao viongozi na wanachama wa Jumuiya hiyo
katika risala yao walieleza jinsi wanavyoshirikiana na kusaidiana katika
nyakati zote hasa pale mara baada ya uchaguzi mkuu uliopita kutokana na baadhi
yao kususiwa katika misiba, harusi na shughuli nyengine za kijamii ikiwa ni
pamoja na baadhi yao kupewa talaka kutokana na msimamo wao wa kuiunga mkono
CCM.
Wanajumuiya hao walimpongeza Mama
Mwanamwema kwa uwamuzi wake wa kuwapongeza na kuzungumza na wanachama na
viongozi hao kutokana na ushindi mkubwa uliopatikana katika uchaguzi mkuu
uliopita huku wakiahidi kuendelea kumuunga mkono Dk. Shein na kumpongeza kwa
hekima, busara, uvumilivu na uwezo
mkubwa alionao katika kuwaongoza wananchi wa Zanzibar.
Wakati huo huo, Mama Shein pia, alikutana na viongozi na wanachama wa
Jumuiya ya (UWT), Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba huko ukumbi wa Kituo
cha Walimu Wingwi.
Mama Mwanamwema Shein katika hotuba yake
alisema kuwa kwa upande mwengine akina mama kupitia umoja wa UWT wanapaswa
kuwapongeza wanawake wenzao wote waliojitokeza kugombania kwani ushindi
walioupata una umuhimu mkubwa kwa maendeleo na ustawi wa wanawake.
Aidha, Mama Shein aliwataka wanawake
kuongeza kasi katika kuunga mkono juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar za kuwawezesha wananchi kiuchumi, hasa wanawake na
vijana.
Alisema kuwa lengo la Serikali ni kuona
wanannchi wanaondokana na changamoto ya utegemezi wa kipato ambapo juhudi hizo,
vile vile zinalengo la kjupunguza na hatimae kuondoa umasikini hapa nchini.
Katika mkutano huo ambao Mama Mwanamwema
Shein alipata mapokezi makubwa, ambapo mapema mke wa Makamo wa Pili wa Rais,
Mama Asha Balozi aliwataka viongozi wakishapata madaraka warudi kwa wananchi
waliowachagua na wakikosa wasiwakimbie na kutowajali.
Nae Mama Fatma Karume aliwataka viongozi
hao kuendelea kukimarisha chama chao pamoja na kuwataka viongozi waliochaguliwa
na wananchi Majimboni kuwasaidia wananchi waliowachagua ikiwa ni pamoja na
kutumia fedha maalum za Majimbo wanazopewa Bungeni na Baraza la Wawakilishi kwa
ajili ya wananchi.
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment