Habari za Punde

Mchezo wac Bonanza Kuchangia Wazee na Watoto Yatima Zanzibar Kati ya Gulioni na Charawe Uliofanyika Uwanja wa Amani Timu ya Gulioni Imeshinda Bao 1-0.

Wazee wa Nyumba ya Wazee Sebleni Zanzibar wakifuatilia mchezo wa Soka kati ya Timu za Gulioni na Charawe uliofanyika Uwanja wa Amaan ulioandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Amani Shein, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ili kuchangia Wazee na Watoto Yatima Zanzibar. Katika mchezo huo timu ya Gulioni kutoka mjini imeifunga Timu ya Kijiji cha Charawe kwa bao 1-0.
 Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibu Unguja Mhe Ayoub Mahmoud akiwasalimia wachezaji wa timu ya charawe kutoka wilaya ya kati unguja.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibu Unguja Mhe Ayoub Mahmoud akiwasalimia na waamuzi wa mchezo huo.kati ya timu ya charawe na gulioni uliofanyika uwanja wa amaan.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibu Unguja Mhe Ayoub Mahmoud akiwasalimia wachezaji wa timu ya gulioni kutoka wilaya ya mjini unguja.
Kikosi cha Timu ya Kijiji cha Charawe iliotowana jasho na timu ya Watoto wa Gulioni mchezo maalum wa kuchangia Wazee na Watoto Yatima Zanzibar uliofanyika uwanja wa amaan usiku. 
Kikosi cha Timu ya Gulioni kilichotoa na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Timu kutoka Charawe Wilaya ya Kati Unguja.











No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.