Habari za Punde

Fundo karibuni kupata umeme

 NAIBU Waziri wa Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Zanzibar Mhe:Juma Makungu Juma, akieleza jambo baada ya kupata maelezo juu ya hali ya upachikaji wa waya za umeme katika nguzo huko katika Kisiwa Cha Fundo Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.(Picha Na ABDI SULEIMAN, PEMBA.)

 VIONGOZI mbali mbali wa Serikali ya Wilaya ya Wete, Wakiongozwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Zanzibar Mhe:Juma Makungu Juma,wakikagua kazi za Uganishwaji wa Umeme katika baadhi ya Nguzo huko katika Kisiwa Cha Fundo Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.(Picha Na ABDI SULEIMAN, PEMBA.)

MAFUNDI wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO Tawi la Pemba, wakiendelea na harakati za kupachika waya za Umeme katika baadhi ya Nguzo zilizoko katika Kisiwa Cha Fundo Wilaya ya Wete, ikiwa ni utekelezaji wa Ahadi ya Rais wa Zanzibar Ifikapo Juni Umeme uwe tayari katika Kisiwa hicho Fundo Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.(Picha Na ABDI SULEIMAN, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.