Habari za Punde

Innaa Lilaahi wainnaa ilayhi Raajiuun, Mussa Soraga hatunaye tena




Mussa Suleiman Soraga ambae ni mjumbe wa wa Kamati Tendaji wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) akiwakilisha ZFA Wilaya ya Magharibi A amefariki dunia saa 12 za jioni ya leo katika Hospitali kuu ya Mnazi mmoja. 

Chanzo cha kifo hicho Marehemu Mussa alipata ajali asubuhi ya leo huko Dole baada ya kugongana Vespa kwa Vespa ambapo moja Vespa hizo yeye alikuwa dereva. 

Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho saa 7 za mchana huko kwao Dole.

ZFA Taifa imepokea kwa masikitiko makubwa kifo hicho cha mjumbe wao wa kamati tendaji. 

Mungu amlaze mahala pema peponi marehemu na amsamehe makosa yake.. Amin

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.