Habari za Punde

Kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar

Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Mgeni Hassan Juma akitoka katika Ukumbi wa Mkutano wa Baraza baada ya kuahirisha Kikoa cha asubuhi kwa mapumziko ya mchana akiongozana na wasaidizi wake na askari wa Baraza.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoka katika ukumbi wa mkutano wa Baraza akiongozana na Mwakilishi wa Nafasi za Rais wa Zanzibar Mhe Ali Juma Khatib (Tadea) wakibadilishana mawazo. 
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakitoka katika Ukumbi wa Mkutano baada ya kuahirishwa kulia Mhe Haroun Ali Suleiman Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi Zanzibar na Mwakilishi wa Jimbo la Tumbe Pemba Mhe. Ali Khamis Bakari 
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakitoka katika ukumbi wa mkutano baada ya kuahirishwa kwa mapumziko ya mchana kulia Mwakilishi wa Jimbo la Mtoni Zanzibar Mhe Hussein Ibrahim Makungu na Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Zanzibar Mhe Mahmoud Thabit Kombo.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu Dawa za Kulevya Zanzibar SACP Kheri Yangu, katikati Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Mihayo Juma Nhunga, wakiwa nje ya ukumbi wa Baraza  baada ya kuahirishwa kwa mapumziko ya mchana. 









No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.