NA HAJI NASSOR, PEMBA
WANANCHI saba wakiwemo wanawake
wawili na wanaume watano, waliounda kikundi cha ufugaji waliopo shehia wa
Ng’ambwa wilaya ya Chakechake, wamekadbiwa Ng’ombe (ndama) saba, kupitia mradi
wa kopa Ng’ombe lipa Ng’ombe.
Hafla
ya makabidhiano hayo, yalifanyika kwenye mabanda ya kufugia Ng’ombe hao yanayomilikiwa
na kikundi cha Umoja ni nguvu cha shehia hiyo.
Mradi
huo wa kopa Ng’ombe lipa Ng’ombe, uliochini ya Mradi wa kuimarisha huduma za
kilimo na mifugo ASSP na ASDP-L unaodhaminiwa na Mfuko wa kimataifa wa
maendeleo ya kilimo ‘IFAD’ kupitia serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kikundi
cha umoja ni nguvu kilikabidhiwa Ng’ombe 20 mwaka 2015 wakiwa na mimba, lengo
baada ya kuzaa majike ni kuwapatia wananchi wenzao ndama hao, ili wafuge na
kisha wengine kuwapa wenzao.
Akizungumza
kabla ya ugawaji wa Ng’ombe hao saba kutoka kwa wanakikundi cha Umoja ni nguvu
kwenda kwa wanakikundi wengine, Mratibu wa mradi huo wa ASSP-ASDP-L Pemba Asha
Omar Faki, alisema lengo ni kuona Ng’ombe hao wanasambaa kwa wananchi wote.
Mratibu
huyo alisema, miongoni mwa masharti ya mradi huo ni kuwa wananchi wafugaji
kujikusanya pamoja, ili kuendesha ufugaji na kisha wanapozaliwa wengine
kuwagawa kwa wengine.
“Huu
mradi lengo lake ni kuona unasambaa kwa jamii yote, baada ya wanaokabidhiwa Ng’ombe
awali wakishazaa, hutakiwa kuwapa wengine ili nao wafuge na baada kuwapatia
wengine kama tunavyofanya leo’’,alifafanua.
Kwa
upande wake mjumbe wa kikundi cha umoja ni nguvu kilichotoa Ng’ombe (ndama) saba,
Said Juma Salim alisema waliyalea makoo hayo 20, waliokabidhiwa ingawa wanne
walikufa baadae.
“Haya
makoo 16 yaliobakia yameshazaa, na leo (jana) tunakabidhi ndama majike saba, kwa wenzetu wafugaji ili nao wakafuge na kisha
kuwapa wenzao’’,alifafanua.
Akizungumza
kwa niaba ya wafugaji wenzake wapya waliokabidhiwa ndama hao, Salama Abdalla
Mohamed alisema, watahakikisha wanawatunza na baada ya kuzaa kuwagawa kwa
wenzao wengine.
“Sisi
tulikuwa na hamu ya kukabidhiwa ndama hawa, maana ufugaji unaweza kututoa
kwenye umaskini nzito tulionao sasa’’,alifafanua.
Mkuu
wa Idara ya Mifugo Pemba Aisha Zaharan Mohamed alisema, wanavyovituo tisa
kisiwani Pemba ambavyo vimeanzishwa na serikali, kwa ajili ya wananchi ili
kujiunga kwenye mpango huo wa kopa Ng’ombe lipa Ng’ombe.
Miongoni
mwa vituo hivyo ni Makundeni, Vikunguni, Mizingani, Piki, Kisiwani, Wingwi na
Makangale ambapo wanavikundi hao, walikabidhiwa Ng’ombe hao tokea mwaka 2015.
No comments:
Post a Comment