Habari za Punde

Mazishi ya Marehemu Mtongori Mang'ache Yafanyika Tarime Mkoani Mara.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tarime, Mchungaji Canon Yohana Chacha (katikati), akiongoza ibada ya mazishi ya Anna Mtongori Mang'ache hii leo katika Mtaa wa Kenyamanyori, halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara.

Wengine ni Mchungaji wa Kanisa la Angilikana Parishi ya Kenyamanyori Tarime, Wyclif Chereme (kulia) pamoja na Mchungaji wa Kanisa Anglikana Parishi ya Kemange Tarime, Charles Mwita (kushoto).

Marehemu Anna Mtongori Mang'ache aliyezaliwa mwaka 1931 Kenyamanyori Tarime, alifariki dunia alihamisi iliyopita Machi 02,2017 katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza.

Familia ya Mang'ache inawashukuru Madaktari wote wakiwemo wa Hospitali ya Winani Tarime, CF na Bugando Jijini Mwanza, jeshi la polisi, viongozi wa dini, ndugu, jamaa na marafiki kwa ushirikiano wao wa dhati katika kumuuguza marehemu Anna Mtori Mang'ache na hata katika kufanikisha mazishi yake. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina!
#BMGHabari
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tarime, Mchungaji Canon Yohana Chacha (katikati), akiongoza ibada ya mazishi ya Anna Mtongori Mang'ache 
Mchungaji wa Kanisa la Angilikana Parishi ya Kenyamanyori Tarime, Wyclif Chereme, akizungumza kwenye ibada ya mazishi hayo
Mwinjilisti Foredy Qojedy, akisoma maandiko ya biblia kwenye mazishi hayo wakati wa ibada
George Binagi akisoma historia fupi ya marehemu kwa niaba ya wanafamilia wakati wa ibada ya mazishi hayo
Wanafamilia wakiwemo watoto wa marehemu Anna Mtongori Mang'che
Kaka wa marehemu, Mzee Maina Binagi, akitoa salamu za familia kwenye mazishi hayo
Wanafamilia wakiuaga mwili wa marehemu
Mwita Mang'ache na Makorere Mang'ache ambao ni miongoni mwa watoto wa marehemu wakiuaga mwili
Mmoja wa watoto wa marehemu, Koplo Thomas Binagi Mang'ache (kulia) na mkewe (katikati) na ndugu, jamaa na marafiki wakiuaga mwili wa marehemu
Kaka wa marehemu, Profesa Lloyd Binagi na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu
Kaka wa marehemu Mzee Chacha Binagi na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu
Kaka wa marehemu Mzee Maina Binagi na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu
Wajukuu za merehemu wakiuaga mwili wa marehemu
Ndugu, jamaa, marafiki pamoja na watoto wa marehemu, wakitoa salamu zao za mwili kwa mwili wa marehemu
Ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wajukuu wa marehemu, wakitoa salamu zao za mwili kwa mwili wa marehemu
Ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wajukuu wa marehemu, wakitoa salamu zao za mwili kwa mwili wa marehemu
Jeneza lenye mwili wa marehemu likipelekwa malaloni
Jeneza lenye mwili wa marehemu likishushwa malaloni
Ndugu, jamaa na marafiki wakirusha udongo malaloni ishara ya kuuaga mwili wa marehemu
Mtoto wa marehemu Mwita Mang'ache na mkewe wakiweka mashada
Mtoto wa marehemu Chacha Mang'ache na mkewe wakiweka shada malaloni
Mtoto wa marehemu na mkwelima wa marehemu wakiweka mashada
Kaka wa marehemu Mzee Maina Binagi na wake zake, wakiweka mashada
Mjukuu wa marehemu akiweka shada
Mtoto wa Marehemu Koplo Thomas Binagi Mang'ache akiwaongoza wajukuu wa marehemu wakiweka mashada
Wajukuu wa marehemu wakiweka mashada
Diwani wa Kata ya Nkende, Daniel Komote, akiweka shada kwa niaba ya viongozi wengine wa siasa
Wanafamilia wakiweka mashada
Familia ya Mang'ache inawashukuru Madaktari wote wakiwemo wa Hospitali ya Winani Tarime, CF na Bugando Jijini Mwanza, jeshi la polisi, viongozi wa dini, ndugu, jamaa na marafiki kwa ushirikiano wao wa dhati katika kumuuguza marehemu Anna Mtori Mang'ache na hata katika kufanikisha mazishi yake. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina!

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.