Habari za Punde

Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe Rashid Ali Juma Akabidhi Uwanja wa Mao Kwa Wajenzi wa Uwanja Huo Kuanza Mradi Huo.

Mchoro wa Uwanja wa Kisasa wa Mao Zanzibar kama unavyoonekana katika picha hiyo jinsi utakavyokuwa baada ya ujenzi wake utachukua miezi 14 hadi kukamilika kwake unaofanywa na Kampuni ya Kichina. 
Hili ndilo eneo la uwanja wa Mao Zanzibar lililokuwa na uwanja miwili wa mpira wa miguu na mpira wa hoki kwa wale waliokuwa na kumbukumbu ya uwanja huu wataufahamu ulivyokuwa kabla ya kuvunjwa kwa majenzo yaliokuweko ndani ya uwanja huu.
Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma akimkabidhi hati ya makabidhiano ya Uwanja wa Mao kwa Muwakilishi wa Kampuni ya Ujenzi wa Mradi huo Ligen Zhang, kutoka China Kampuni ya Zhengtal Group Limeted hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika viwanja vya uwanja huo Mao Tse Tung Zanzibar leo.akishuhudia Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Ndg Omar Hassan King katikati.  
Waziri wa habari Utalii Utamaduni na Michezo Mhe Rashid Ali Juma akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi uwanja huo kwa Mkandarasi leo katika viwanja vya mao.
Msimamizi wa Ujenzi huo kutoka Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na MichezoNdg Ali Mbarouk akizungumza na waandishi wa habari jinsi ya uwanja huo utakavyokuwa katika kukamilika kwa Mradi wa Ujenzi huo wa Uwanja wa Kisasa na  wa aina yake kwa Zanzibar na Afrika Mashariki. utakuwa wa mfano.  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.