Awataka wawe
waangalifu na kazi zao
NA HAJI
NASSOR, PEMBA
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk: Ali Mohamed Shein, amewataka
wakandarasi na washauri elekezi kwenye majengo ya serikali, kuwa makini na kazi
zao, kwani fedha zinazotumiwa ni za wananchi, hivyo hazihitaji kuchezewa.
Alisema lazima waelewe kuwa, kila
jengo la serikali linalojengwa, zinazotumika huwa ni fedha za walipa kodi,
hivyo lazima wawe makini ikiwa ni pamoja na kufuata wakati wa ujenzi na
umaliziaji, uliomo kwenye mikataba yao.
Dk: Shein alieleza hayo Daya Mtambwe
Wilaya ya Wete Pemba, mara baada ya kupokea maelezo ya kukinza kutoka kwa
mjenzi na mshauri elekezi, wanaojenga Chuo cha Amali kilichopo eneo hilo, ikiwa
ni sehemu ya ziara yake ya siku tano kisiwani humo.
Alisema hata kama jengo hilo
linajengwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika ADB, lakini
itafika wakati mkopo huo unahitajika kulipwa kwa fedha za walipa kodi wa ambo
ni waaanzibari.
Alieleza kuwa, ujenzi huo ambao
alisema takriban umesimama kwa miezi saba, alikuwa na hamu ya kufika eneo hilo,
ili kujionea kwa macho yake, na kujua sababu za kusimama kwa ujenzi huo.
Hivyo amewataka wajenzi ambao ni kampuni
ya ZECCON LTD chini ya mshauri elekezi Mohamed Nuren kutoka kampuni ya Newtech
Consulting Group ya Sudan, kufikia mwafaka wa haraka, ili jengo hilo
lililofikia hatua ya msingi, lijengwe na limalizike kwa wakati.
Dk: Shein alieleza kuwa, jengo hilo
linasubiriwa kwa hamu na wananchi, ili walitumie kwa maslahi ya kupata ujuzi na
kisha kuwa na njia za kujikwamu na umaskini.
“Mimi nilikuwa na hamu ya kuja kuona
mwenyewe, na nimeshayasikia melezo ya pande zote mbili, nimeridhika na fanyeni
haraka kuendelea na ujenzi, walu mwakani likamilike’’,alifafanua.
Akizungumza na wanafunzi wa skuli ya
Daya Mtambwe mara baada ya kupokea maelezo kwenye jengo hilo la chuo cha Amali,
amewataka kuacha anasa na kusoma zaidi, ili wajenga msingi madhubuti wa maisha
yao ya baadae.
Alisema lazima wanafunzi katika
kipindi hichi, wajielewe kuwa kazi ilioko mblele yao, ni moja tu nayo ni
kuwatii wazazi na walezi wao, huku wakisaka elimu kwa hali yoyote.
“Acheni kila jambo lisilo na maslahi
na sasa kazi yenu nyinyi ni kusoma na serikali yenu inaendelea kujenga chuo cha
amali ili wengine mnaweza kujiunga na kutafuya ujuzi’’,alifafanua.
Dk: Shein aliwakumbusha wanafunzi hao
pamoja na wananchi wengine kuwa, ujenzi wa chuo hicho cha amali, alikidahidi
mwaka 2010 wakati akiwa kwenye kampeni zake za kuomba kuchaguliwa kuwa rais.
“Kile nilichokiahidi kupitia Ilani ya
chama cha mapinduzi ya mwaka 2015 hadi 2020, leo nakitekeleza kwa vitendo, sasa
kazi yenu kikimalizika tuni kusoma kwa
bidii na kuchota ujuzi ’’,alifafanua.
Mapema Ali Mbarouk Juma kutoka
kampuni ya ZECCON LTD ya Zanzibar, alimueleza rais huyo wa Zanzibar kuwa,
kilichosababisha kusita kwa ujenzi wa jengo hilo, ni kutofanyiwa vipimo vya
kitaalamu udongo wa eneo hilo.
“Mheshimiwa tatizo lililojitekeza
hapa, huu udongo mwengine haukufanyiwa vipimo, ingawa kwa sasa tayari na wakati
wowote ujenzi utaendelea’’,alisema.
Awali Rais huyo wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na ujumbe wake, ulifika eneo la
Mzambarau takao na kupokea taarifa ya ukarabati wa barabara ya Madenjani hadi
Mzambarau takao.
Dk: Shein alipongeza hatua iliofikwa ya
ukarabati wa barabara hiyo, kazi inayofanywa na kampuni ya MECCO ya Tanzania
bara, inayoendelea na kuwataka kukamilisha kwa wakati.
“Sawa mimi nimefurahi na nimeona kazi
yenu ya ukarabati wa barabara hii, endeleeni na jitahidini mmalize kwa wakati,
ili wananchi wapate kuitumia kwa upana’’,alishauri.
Dk Shein yupo kisiwani Pemba kwa
ziara ya siku tano, ambapo pamoja na mambo mengine, anatarajiwa kutembelea
ujenzi wa barabara ya Ole- Kengeja, kuzungumza na waalimu wa skuli za
sekondari, barabara ya Kipapo- Mgelema, Kuyuni- Ngomeni pamoja na kuzungumza na
kamati za chama kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment