Habari za Punde

Kampuni ya Simu ya Vodacom Limited Inauza hisa (share) Zake Kupitia Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ Bank)


BENKI YA WATU WA ZANZIBAR
·         Kampuni ya simu ya Vodacom Limited inauzahisa (share) zake kupitia Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ Bank) kwa shilingi 850/- kwa hisa moja. Hii fursa pekee kwa wananchi wote wa Tanzania kuweza kuwekeza katika kampuni hio.
·         Hisa hizo zita uzwa kuanzia tarehe 09/03/2017 hadi tarehe 19/04/2017 (Kwa kipindi cha wiki sita).
·         Kiwango cha mwanzo cha manunuzi ni hisa (share) 100 kwa thamani ya shilingi 85,000 na anaweza kuongeza hisa 10, 10 kwa thamani ya shilingi 8,500/- kwa kila nyongeza.

·         Kwa ajili ya ununuzi, utatakiwa kufanya malipo kwenye account ya ZanSecurities Limited yenye nambari 06107000074 iliopo Benki ya Watu Wa Zanzibar (PBZ Bank). 
·         Baada ya kufanya malipo utajaza fomu maalumu ya kununulia hisa kulingana na kiwango cha fedha zako ulizolipa.
·         Kwa maelezo Zaidi tafadhali fika kwenye tawi la Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ Bank) liliopo karibu yako.

PBZ BANK: BENKI YA WATU, CHAGUO LA WATU



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.