Na Mwandishi wetu
Mkuu
wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Omar Khamis Othman amefanya uteuzi wa masheha
wapya pamoja na kuongeza idadi ya shehia mpya katika mkoa huo.
Katika taarifa yake kwa
vyombo vya habari ni kwamba uteuzi huo umefanyika baada ya serikali ya mkoa
kupokea ushauri kutoka Wilaya uliozingatia uwezo wa mtu kutendaji .
Aidha kwa mujibu wa sheria
no 8 (1) cha sheria no 8 ya mwaka 2014, ambayo imempa nguvu kisheria Mkuu wa Mkoa kufanya uteuzi wa masheha katika eneo lake.
Masheha
wapya walioteuliwa ni, Ali Khatib Chwaya ameteuliwa kuwa sheha wa Shehia ya
Sellem, Ramadhan Omar Ahmed Shehia ya Kipange, Mwanaidi Khamis Alela Shehia ya
Maziwani na Shabaan Salim Mtwana kuwa Shehia ya Kisiwani kwa Binti Abeid.
Wengine
ni Ali Khalid Ali Sheha wa shehia ya Mzambarau Takao, Mariam Juma Ali shehia ya
mlindo , Said Othman Kombo Shehia ya Chamboni , Ali Hamad Sharif Shehia ya Shanake
Faki Kombo Hamad Shehia ya Majenzi pamoja na Khatib Hamad Mbwana ambaye
ameteuliwa kuwa sheha wa Shehia ya Kiuyu.
No comments:
Post a Comment