Dar es Salaam,
Katika
kuleta ufanisi na ubunifu kwenye sekta ya Mawasiliano, ambayo imeleta
mabadiliko kwenye maisha ya mamilioni ya Watanzania, Kampuni ya mawasiliano
Zantel imeendelea kuboresha huduma za kisasa za mtandao wake ili kuhakikisha
wateja wao wanazidi kufurahia huduma ya mtandao wenye kasi wa 4G.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini
Dar es Salaam, Mkurugenzi mkuu wa Zantel Bw. Benoit
Janin amesema “Mchakato wa kuboresha mtandao wa Zantel visiwani Zanzibar na
Tanzania Bara umekua ukiendelea vizuri, kuhakikisha wateja wetu wanaendelea
kufurahia manufaa ya teknolojia ya simu kupitia mtandao wa simu wa Zantel.”
Uboreshaji unaoendelea utaweza kuhimarisha zaidi ubora wa
mtandao wetu, huduma za intaneti za kasi zinazotumiwa zaidi kwa sasa sokoni na
wateja ni hii ya 4G.”
Aidha, aliongeza kwa kusema, Uboreshaji wa maeneo yote ya Stone
Town na mikoa ya Magharibi umefanikiwa. Zoezi la kuendelea kuboresha huduma
hizo kwa visiwa vya Unguja na Pemba linaendelea na litakamilika ifikapo Mei
mwaka huu.
Mradi mzima utagharimu zaidi ya dola za kimarekani milioni 10
hadi kukamilika. Mtandao wa Zantel utaweza kutoa huduma bora zaidi kwa wateja
wake, pamoja na mtandao utakaowafikia zaidi ya asilimia 85 ya Watanzania wanaotumia
huduma za simu ya mkononi zenye ubora zaidi, intaneti yenye kasi pamoja na
kuboresha huduma za fedha.
Amesema mradi una lengo kufanya mabadiliko kwenye vituo vyote
vya huduma za katika mitandao ya simu kwa kisiwa cha Zanzibar na Tanzania Bara
kwa kufunga vifaa bora vya kisasa.
Mtandao wa Zantel unawakaribisha Watanzania wote kutumia na
kufurahia huduma ya intarneti ya 4G kutoka Zantel kama kampuni ya mtandao wa
simu ya kwanza kuleta huduma za kibenki kwa jamii ya Kiislamu na kwa nchi
nzima.
Kuhusu
Zantel
Mtandao wa Mawasiliano wa Zanzibar (Zantel) ni
miongoni mwa wawekezaji na wagunduzi kwenye sekta ya mawasilino wakiongoza kwa
utoaji wa huduma bora kwa wateja. Lakini zaidi ya yote, ni miongoni mwa kampuni
ya mawasilino inayokuwa kwa kasi kubwa na inayotengeneza faida kubwa katika
Sekta ya mawasiliano Tanzania. Mtandao huu wa Mawasiliano Zanzibar ndiyo
mtandao pekee wa huduma za mawasilino unaotoa huduma ya simu za nje kwa bei
nafuu, simu nab ado kupitia mfumo bora wa CDMA, GSM, 3G networks.
Huduma za Zantel zimekuwa zikikua kutokana na
kuongezeka watumiaji wake huku ikizidi kuonyesha ubora katika huduma zake
ambazo kila mtu anaweza kuzimudu pamoja na kutoa huduma ya haraka ya mtandao wa
wireles kwa haraka na ubora.
Zantel imepokea tuzo mbalimbali kutokana na
kutambuliwa kutoa huduma bora na ufumbuzi kwenye sekta ya mawasilino. Baadhi
yake ni pamoja na Tuzo ya GSMA M – Health. Zantel imedhamiria kuwaunganisha
watu ulimwenguni ili wawe mstari wa mbele kupata tarifa kwa haraka.
Kwa maelezo zaidi tafadhali, tembelea mtandao wetu…www.zantel.com
No comments:
Post a Comment