Habari za Punde

Tatu Abdalla Msellem, jasiri wa uongozi ndani ya Jumuia


- Aanika matamu, machungu ameshawahi kuvamia jimbo

 NA HAJI NASSOR, PEMBA

KUTOKANA na umahiri wangu wa kazi na kutekeleza vyema majukumu yangu, ndio maana nikachaguliwa na kupewa hii nafasi.

Nasema haya sikama najisifu, au kutaka sifa na kujinyoonesha kwa watu kama nayaweza, lakini nasema haya kwa kujiamnini, na walio wengi wanaamini kama kweli mimi najiamini na naweza.

Hizo ni baadhi ya kauli za mwanamke mahiri ambaye anaoneka kweli anaweza na anajiamini.

Jina lake hasa ni Tatu Abdallah Msellem, aliyeshika wadhifa wa Mwenyekiti katika Jumuiya ya ‘Tumaini jipya’ TUJIPE kisiwani Pemba.

Mwanamke huyu mahiri, ana historia ndefu katika maisha yake, licha ya kuwa amejinyakulia wadhifa huo bila ya yeye mwenyewe kujua.

Kitu pekee kilichosababisha kujinyakulia wadhifa huo, ni kutokana na kujiamini kwake katika utendaji wa kazi na majukumu yake.

Ama kweli…. wanawake laiti kama sikujengewa, misingi potofu na ya kuwakandamiza leo, tungewakuta kama Bi Tatu wapo kwa wengi.

Jumuia hii ‘Tuamini jipya’ anayoingoza mwanamke huu, ikiwa na akina baba 15, ilianza kazi zake, mwaka 2008 na kupata usajili mwaka mmoja baadae.

‘’Lengo hasa la kuanzishwa kwa Jumuiya hii ni kustawisha na kuimarisha maendeleo endelevu ya wanajamii wa Pemba katika nyanja zote’’, alilieleza lengo.

Bi Tatu akiwa muanzilishi wa Jumuia hiyo, waliamua kuanzisha huku wakiamini kuwa, inaweza kusaidia kwa njia moja au nyengine, ili kuweza kuisadia jamii.

Jumuiya ilianza ikiwa na wanachama 13, lakini kutokana na umahiri wa Mwenyekiti wake mwanadada huyu, kwa kushirikiana na wenzake waliitangaza hadi sasa kuwa na wanachama 32.

Ama kweli, ile kauli isemayo wanawake wanaweza, haikwenda kombo…………kwa mweneyekiti huyu.
Wanaume waliowengi wanaamini kuwa nafasi kama ya 

Mwenyekiti, Katibu na hata msaidizi Katibu, hushikwa na wanaume, ambapo kwa ndani ya Juamuia hii mambo ni tofauti.

 ‘’Muda mwingi naupoteza nikiwa katika harakati za jumuiya huku nikizingatia kazi hizi ni kujitolea zaidi, unachokipata ni kidogo mno’’, alisema Mwenyekiti.

Tatu Abdalla Mselemu, ni mwanamke anaewawakilishi wanawake wengine kadhaa wa kisiwa cha Pemba, na kuwaonyesha wale wanaume wanaodhani kuwa mwanamke hawezi kuongoza nafasi za juu.

Mmoja wa wasioamini kuwa mwanamke angeweza kuongoza kwenye nafasi kama hiyo ni Katibu wa Jumuiya hiyo bw: Ali Suleiman Khamis, yeye hapa alisifu juhudi zinazochukuliwa na Mwenyekiti wao.

‘’Unajua kweli mwanamke anaweza tena hata kama hakuwezesha, chamsingi ni kujengewa mazingira bora, na anaebisha aje kwenye Jumuia yetu, yupo mama mahairi Tatu Abdalla’’,anasema.

Yeye haamini mambo anayoyafanywa Mwenyekiti wao, kupitia Jumuia hiyo na wamefika pahala hata kwenye uchaguzi wa mara ya pili mwaka 2011 walimpitisha kwa kura nyingi.

Inawezekana karne kadhaa zilizopita wanawake walionekana si chohochote, na ndio maana walikosa kutumia haki yao ya kuongoza, na leo wapo wanaokuja juu.

‘’Kwa kweli Jumuiya nzima inamuamini Bi Tatu kutokana ukakamavu wake wa kazi zake,  kiasi ambacho huweza kufanya kitu sisi wanajumuia hatuwezi kuamini’’, alidakiza Suleiman Makame Issa ambae ni mshika fedha.

Mshika fedha huyu  aliweka bayana kuwa, walimchaguwa mwanama huyo aliezaliwa miaka 41 iliopita,  kwa kura nyngi za ndio, kutokana na umahiri wake.

Unaweza kushangaa, Mwenyekiti huyu wa Jumuia ya tumaini jipya, kwamba huku ni mfanyakazi wa serikali, wakati huo akiwa na asasi ya kimaendeleo.

‘’Walishsema wahenga………. haba ba haba hujaza kibaba, na msemo huu kwake aliujibu kutokana na maisha kwa sasa kumuelemea kila mmoja’’.

Mwenyewe ansema kuwa, hapendi kuona jamii hasa kwa yale makundi yaliotajwa kuwa yako pembezoni, kukosa haki zao kama vile za kujiamualia mambo yao na ndio maana lengo moja la jumuia yake ni kuwakomboa .

‘’Mimi niliishauri kamati yangu tendaji kabla hata ya kupata ufadhili, tuende baadhi ya vijiji kukutana na wajane kuwapa elimu na hili lilipita’’,alisema kwa ukakamavu.

Uchesi na ukakamvu wa mwanamama huyu, amekua kama chumvi ndani ya Jumuia yake, kutokana na kila anachokieleza, hukubalika na kisha kuzaa matunda.

Majukumu ya Mwenyekiti huyu ni sawa na yale ya Mwenyekiti mwengine hata akiwa mwanamme, katika Jumuia nyengine, ingawa zipo asasi za kirai kutokana na kurithi mifumo dume, huwakosesha nafazi wanawake.

 ‘’Mimi majukumu yangu hasa katika Jumuiya, ni kuhakikisha Jumuiya inatimiza malengo yake kama ilivyojipangia katika katiba’’, alifahamisha Bi Tatu.

Jukumu jengine na kubwa ni kutekeleza kazi nyengine za Jumuiya, kama atakavyopangiwa na kamati Tendaji na mkutano mkuu.

Miaka hiyo akiwa skuli alidhani suala la uongozi ni zito na hata kutafsiri kwamba, asingeweza chohote hata kama akipewa nafasi.

Leo mwanamke huyu ambae pia ni mfanyakazi wizara ya habari Kisiwani Pemba, anajivunia kuongoza kundi kubwa la wanaume kwa ufanisi.

Kutokana na umahiri wa Mwenyekiti tayari Jumuiya walishapata mradi mmoja wa mafunzo ya utunzaji wa fedha uliofadhiliwa na Foundation for Civil Socierty.

‘’Mradi huu ulikuwa wa miezi mitatu, uligharimu shilingi milioni saba (7,000,000) na wanachama 15 wakiwemo na wajumbe wa kamati tendaji, walipatiwa mafunzo ’’, alieleza Mwenyekiti.

Bi Tatu ambae ni mwenyeji wa kijiji cha Ng’ambwa kilichopo Wilaya ya Chakechake tokea mwaka 1975, tayari ameshajinyakulia digirii yake ya masuala ya biashara na fedha.

‘’Nilianza kusoma skuli darasa la kwanza nikiwa na umri wa miaka sita mwaka 1981, katika skuli ya msingini ya Chachani ‘’, alisema Mwenyekiti.

Kwa elimu ya sekondari, Bi Tatu alilazimika kubadili mazingira na kuelekea skuli ya Shamiani, ndani ya mwaka 1989 na alimaliza hapo mnamo mwaka 1992.

‘’Baada ya kumaliza masomo yangu mwaka huo, niliamua kusomea ualimu ngazi ya cheti chuo cha uwalimu Mkurumah Unguja kuanzia mwaka 1999, hadi kufikia mwaka 2001’’,alieleza .

Baadae aliajiriwa na serikali, kupitia wizara ya elimu, akiwa kama Sekretary, ingawa baadae alianza kazi ya kusomesha.
 ‘’Nilisomesha Pujini msingi kwa miaka mitatu na hapo ndipo nilipopata uhamisho na kupelekwa skuli ya msingi ya Ole na hapo nilisomesha kwa muda wa miaka kumi’’, alifafanua.

Kabla ya kuikwaa nafasi hii ya Mwenyekiti Bi Tatu alishawahi kuwa mjumbe wa bodi ya wadhamini, kupitia Jumuiya ya Waganga wa jadi kisiwani Pemba.

 Licha ya kuwa Jumuiya inaenda vizuri katika kuendesha shuhguli zake, lakini kuna changamoto mbali mbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vitendea kazi.

Afisa katika kamati tendaji wa Jumuiya hiyo, Hamad Hassan Chande alimsifia sana mwanadada huyo, na kusema kuwa ni kiongozi jemedari ndani ya Jumuiya.

Wapo wengine waliomsifia Bi Tatu, akiwemo Hadhifa Omar Khamis, anasema kama katiba yao haikutoa maelekezo ya kubadilishana uongozi, basi Mwenyekiti wao engeendelea daima.

“Mimi wakati sijamjua sana niliona ni wale wanawake wa mwaka 1972, wa hewalwa bwana, kumbe yeye ni shujaa alietimia kwenye uongozi’’,alisema.

Pamoja na mafanikio hayo mwanadada huyo kwenye suala la uongozi, anakula changamoto kadhaa kama vile wanajumuia yake kuwa na uwelewa mdogo wa mambo kadhaa.

Jengine lililozaliwa na hilo ni kujikuta akibeba majukumu mengi kwa wakati mmoja ya Jumuia, ingawa huyamudu.

Nae kama walivyobinaadamu wengine, amejipangia malengo yake katika safu ya uongozi, kugombania Ubunge kwa vile anatamani sana kuona wananchi Pemba wamepiga hatua kubwa ya kimaendeleo.

Anatamani kesho asubuhi iwe ndo mwaka 2020 ili ajitupe tena jimboni kwa mara ya pili, maana mwaka 2015 aliingia katika Jimbo la Ole ingawa hakufanikiw akuingia Dodom.

“Sijafa moyo kuingia tena jimboni, na mara hii mwaka 2020 ikifika tu, kama kawaida nachukua fomu na kupanda juu ya kiriri kuomba kura’’,anasema.

Mwanake Asha Bakari Juma anasema wanawake aina ya Tatu ndio haswa wanaofaa kuungwa mkono kutokana na kuoyesha moyo wa uzalendo.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mwanajuma majidi Abdalla akizungumza kwenye siku ya wanawake duniani ukumbi wa kiwanda cha Makonyo alisema, kila mwanamke anayo haki ya kuwa kiongozi.

“Mimi si nipo hapa kwenye nafasi ya mkuu wa mkoa na nip eke yangu kwa Zanzibar, sasa na nyinyi fikeni pahala msiwaachie wanaume pekee’’’,alifafanua.

Sheikh Daud Khamis Salum wa ofisi wa Mufti Pemba anasema hakuna kipengele ndani ya uislamu kilichomkataza mwanamke kugombea uongozi.

“Mwanamke anayohakia na wajibu wa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi  ndani ya jamii, kama nafasi anayo dini haimkatazi’’,anaeleza.

Mzuri Issa kutoka TAMWA anasema wamekuwa wakiwahamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi na sio tu kwenye jumuia hata majimboni.
                             









No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.