GARI aina ya kijiko kikiondoa udongo
ulioporomoka na kuvunja ukuta wa ghala la kuhifadhi karafuu Mkoani, kufuatia
mvua inayoendelea kunyesha na kusababisha karafuu zilizokuwemo kuathirika, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
KATIBU Mkuu wizara ya Nchi Afisi ya Makamu
wa Pili wa rais Zanzibar Joseph Abdalla Meza (katikati) akizungumza na Mdhamini
wa ZSTC Pemba Abdalla Ali Ussi, kufuatia ghala la kuhifadhia karafuu Mkoani
kuvunjika kwa kuelewa na mlima, kipindi hichi cha mvua zinazoendelea kunyesha, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
KULIA ni Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Hemed
Suleiman Abdalla, akielezea athari za mvua zilizojitokeza wilayani mwake, kwa
Katibu Mkuu wizara ya Nchi Afisi ya
Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Joseph Abdalla Meza (katikati) wakati alipokuwa
na ziara ya kuyatembelea maeneo na nyumba za wananchi waliokumbwa na athari za
mvua, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MLIMA uliokaribu na ghala la kuhifadhi
karafuu Mkoani, ambao uliporoka wiki iliopita, na kusababisha athari kwa
kukatika ukuta wa ghala hilo, na karafuu zilizokuwa zimehifadhiwa kuharibika, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
KATIBU Mkuu wizara ya Nchi Afisi ya Makamu
wa Pili wa rais Zanzibar Joseph Abdalla Meza, mwenye mwemvuli akiangalia nyumba
na msikiti ulivyokumbwa na athari ya kuelemewa na mlima, shehia ya Mbuyuni wilaya
ya Mkoani Pemba, wakati wa ziara yake ya kuyatembelea maeneo na nyumba za wananchi, zilizoathiriwa na mvua,
kushoto ni mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MSIKITI wa waumini wa shehia ya Mbuyuni
wilaya ya Mkoani Pemba, ambao ni miongoni mwa majengo yaliokumbwa na athari za
mvua, kwa kuangukiwa na mlima na kisha tawi la mti, ambapo kwa sasa umehamwa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MITI ya aina mbali mbali ikiwemo
mikarafuu, mifenesi, migomba na misheli sheli inayomilikiwa na wananchi wa
kikiji cha Kwachangawe wilaya ya Mkoani Pemba, ikiwa imekatika katika, kufuatia
upepo wa kasi uliovuma juzi Mei 8, pia ulisababisha nyumba sita kupata athari, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MKUU wa wilaya ya Mkoani Pemba Hemed
Suleiman Abdalla, akimuonyesha miti iliokatika kwa upepo eneo la Kwachangaawe
wilayani humo, Katibu Mkuu wizara ya
Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Joseph Abdalla Meza, wa pili
kulia, wakati Katibu mkuu huyo na ujumbe wake ulipoyatembelea maeneo kadhaa ya
wananchi yalioathirika na mvua, (Picha
na Haji Nassor, Pemba).
NYUMBA inayomilikiwa na mwananchi Salim
Saleh Mbaruok wa Kwachangaawe wilaya ya Mkoani, ikiwa imepata athari kufuatia
upepo wenye kasi, uliovuma juzi na kusababisha wananchi sita nyumba zao kuharibika,
(Picha na Haji Nassor, Pemba).
No comments:
Post a Comment