Mwandishi wa habari hii wakati akimuhoji mmoja wa wajariamali wadogowadogo
Na Ali Ngome Ali, Pemba
Wajasirimali wadogo wadgo Kisiwani Pemba wameiomba Serekali kuendelea kuwapatia elimu ili kuweza kukuza mitaji yao.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizri mapema leo hii wajasiriamali hao wamesema kuwa kupatiwa nafasi za kushiriki katika mafunzo mbali mbali kunawezesha kujenga uzoefu wa biashara wanazozifanya nakuweza kujikwamua hali ngumu za kimaisha.
Amefahamisha kuwa kupitia mradi wa GAWE umemuwezesha kujua kutunza kumbukumbu jambo ambalo awali hakuweza kufikiria kabisa juu ya utunzaji huo.
Nae Fatma Khamis Ameir Mkaazi wa Wete amesema ipo haja kwa wajasiria mali ambao wemepata mafunzo kuweza kuyatumikia vyema kwa lengo la kuimarisha biashara zao nakuondokana nadhana yakuwa mafunzo niyakujipatia fedha pekee.
Aidha ametoa wito kwa wajasiriamali kutokuvunjika moyo nabadalayake kujiendeleza na kuondokana na hali ngumu ya kimaisha huku wakijua biashara nikitu gani jambo ambalo litamuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
No comments:
Post a Comment