Na.Haji Nassor - Pemba.
MWENYEKITI
wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali Bakari, amesema sheria
ijayo ya kudhibiti uharibifu wa mazao, itawabana pia masheha wenye tabia kutoa vibali
kwa wafanyabiashara, wanaosafirisha mazao machanga au yalioivishwa kwa moto
ikiwemo ndizi.
Alisema kwa sasa sheria hiyo inaendelea kufanyiwa
mapitio na tume yake kwa kuwashirikisha wadau mbali mbali, hivyo ndani ya
sheria hiyo vimo vifungu vinavyowagusa viongozi hao wa shehia iwapo watatoa
vibali kiholela.
Mweyekiti huyo alieleza hayo kwa nyakati tofauti
wakati akizungumza na msheha wa mkoa wa kaskazini Pemba pamoja na wadau,
wengine wakati akifungua mkutano wa uwasilishaji wa rasimu za awali za sherioa
za uharibifu wa mazao, sheria ya usajili wa nyaraka na urithi wa ardhi endelevu
mkoani humo.
Alisema kwa sasa wapo wafanyabiashara wamekuwa na
mfumo wa kuyaharibu mazao ikiwa ni pamoja na kuyachuma machanga au kuyaivishia
kwa moto bila ya kuulizwa, ingawa sheria inayokoja hilo litahesabika kama kosa.
Aidha Mwenyekiti huyo wa tume ya kurekebisha sheria,
alisema hata masheha kama wakijaribu kuwapa vibali vya kusafirishia
wafanyabiashara wenye tabia hiyo, nao sheria inawamulika hivyo lazima wajitenge
na jambo hilo.
Katikati
ni Jaji Mshibe Ali Bakar, ndie Mwenyekiti wa Tume hiyo
“Sheria hii ambayo ni kongwe na sasa inafanyiwa
marekebisho, haitowagusa tu waharibifu wa mazao kama vile wafanyabiashara
waoingiza au kutoa nje ya Zanzibar mazao, hata masheha wakitoa vibali kw
amuharibifu nao watawajibika”,alifafanua.
Katika hatua nyengine Mwenyekiti huyo, aliitaja jamii
kuendelea kujenga utamaduni wa kusajili nyaraka zao pamoja na ardhi ili ziwe na
thamani kisheria.
Mapema Katibu wa Tume hiyo Asma Hamid Jidawi, alisema
sheria ya usajili wa ardhi endelevu, unalengo pia la kuondoa migogoro kwenye
ardhi za matumizi endelevu kama vile viwanja wa michezo, misikiti na makanisa.
Baadhi ya masheha wa mkoa wa kaskazini Pemba, walisema
kama sheria hiyo itatekelezwa ipasavyo baada ya kupitishwa yaweza kuwa ni
mwarubani wa mazao kununuliwa yakiwa na uasili wake sokoni.
Sheha wa shehia Micheweni Dawa Juma Mshindo alisema
Zanzibar inazosheria nyingi na mzuri, ingawa changamoto huja kwenye utekelezaji
wake.
Akiswalisha mswada wa sheria ya usajili wa nyaraka
mwanasheria kutoka tume hiyo Mwita Khamis Haji, alisema sheria hiyo imeeleza
aina mbili za nyaraka zikiwemo za lazima na nyengine ambazo ni hiari.
“Nyaraka ya nyumba unayoishi au wa kiwanja cha nyumba
hizi ni lazima, ingawa zipo nyengine kama vile mikataba ya kijamii hizi
hulazimiki, ingawa faidi yake ukizisajili zipo”,alisema.
Tume ya
Kurekebisha sheria Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake jaji Mshibe Ali Bakar
imeshazifanyia marekebisho sheria 17 ikiwemo sheria ya ushahidi, sheria ya
wanyama, vileo na sheria ya usafirishaji baharini, na kwa sasa wanaendelea na
sheria za uharibifu wa mazao, nyaraka na ardhi endelevu.
No comments:
Post a Comment