Habari za Punde

Afariki baada ya kuangukiwa na gogo la mti

Na Said Abdulrahman,  Pemba
MTU mmoja amefariki dunia baada ya kuangukiwa na Gogo la mti huko Machengwe,Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Akithibitisho kifo cha marehemu huyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Haji Khamis Haji, alimtaja marehemu kuwa ni Suleima Juma Khamis (47) mkaazi wa Utaani Wete.
Alifahamisha kuwa tukio hilo lililokea hapo jana majira ya saa 11:30 za jioni huko katika bonde la Machengwe Wilaya ya Wete.
Alieleza  kuwa marehemu alipatwa na kifo hicho akiwa katika shughuli zake za kukata mti aina ya mfuu kwa ajili ya kupigia tanu kwani ni kazi yake maarufu   aliyokuwa akifanya marehemu huyo.
“Ni kweli hapo jana majira ya saa 11;30 za jioni, kuna huyu Suleiman Juma Khamis, mkaazi wa Utaani alipatwa na kifo baada ya kuangukiiwa na gogo la mfuu wakati akijaribu kuutaka huko katika bonde la Machwengwe,”alisema Kamanda Haji.
Alisema kuwa chanzo cha kifo cha marehemu huyo ni kuangukiwa na na gogo hilo ambapo    mti huo ulikosa muelekeo na kugonga mnazi na baadae kumuangia   ambapo marehemu aliumia sehemu za mdomoni.
“Kwa mujibu wa maelezo daktari aliemfanyia uchunguzi ,alisema kuwa marehemu huyo aliumia katika sehemu za mdomoni ambapo gogo hili lilipiga,’alifahamisha Haji.
“Wito wangu kwa wananchi kuacha tabia ya kufanya kazi mtu mmoja mmoja hasa wale wavuvi pamoja na hawa ambao wanakata miti kwa ajili kujitafutia riziki,”alisema Kamanda Haji.

Hivyo alisema iwapo Mtu atafanyakazi kama hizo akiwa na wenzake, wanaweza kusaidiana  hata ushauri na kuepusha majanga kama hayo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.