Habari za Punde

Rais Dk Shein azungumza na bodi ya wakurugenzi wa ZBC, Uongozi wa Wizara ya Habari, Utalii na Michezo

 Mwenyekiti wa Bodi ya  Wakurugenzi ya ZBC Bi.Nasra Mohamed (kulia)  alipokuwa akitoa taarifa ya Bodi yake  wakati wa kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,ambacho kilijumuisha Uongozi wa Wizara ya  Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo na Uongozi wa ZBC, chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),(kushoto) Mjumbe wa Bodi Nd,Ali Bakari,  [Picha na Ikulu.] 09 /08/2017.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo , Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZBC pamoja na Uongozi wa ZBC leo   katika kikao cha siku moja kilichofanyika katika  Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja, [Picha na Ikulu.] 09/08/2017. 
 Mkurugenzi Mkuu wa ZBC Nd,Iman Othman Duwe (kulia) alipokuwa akitoa maelezo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)  katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo  katika kikao cha siku moja cha  Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,Bodi ya Wakurugenzi ya ZBC na Uongozi wa ZBC,ambacho kikao hicho kimejadili mambo mbali mbali ya kiutendaji ya ZBC na Bodi kwa pamoja,(kushoto) Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi Serikalini Mhe.Mohamed Fakih, [Picha na Ikulu.] 09 /08/2017. 



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.