Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZBC Bi.Nasra Mohamed (kulia) alipokuwa akitoa taarifa ya Bodi yake wakati wa kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,ambacho kilijumuisha Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo na Uongozi wa ZBC, chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),(kushoto) Mjumbe wa Bodi Nd,Ali Bakari, [Picha na Ikulu.] 09 /08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo , Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZBC pamoja na Uongozi wa ZBC leo katika kikao cha siku moja kilichofanyika katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja, [Picha na Ikulu.] 09/08/2017.
Mkurugenzi Mkuu wa ZBC Nd,Iman Othman Duwe (kulia) alipokuwa akitoa maelezo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo katika kikao cha siku moja cha Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,Bodi ya Wakurugenzi ya ZBC na Uongozi wa ZBC,ambacho kikao hicho kimejadili mambo mbali mbali ya kiutendaji ya ZBC na Bodi kwa pamoja,(kushoto) Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi Serikalini Mhe.Mohamed Fakih, [Picha na Ikulu.] 09 /08/2017.
No comments:
Post a Comment