Skuli ya Maandalizi na Msingi ya Highlight , ilipo Wawi Chake Chake Pemba.
Picha na Bakar Mussa -Pemba.
Na Bakar Mussa-ZANZIBARLEO.
Mkurugenzi
mkuu wa Skuli ya Maandalizi na Msingi ya Highlight, ilioko Wawi Chake Chake
Pemba, Hamad Bakar Ali, ameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar , kuunga mkono
juhudi zilizochukuliwa na Uongozi wa Skuli hiyo katika kuinuwa kiwango cha
Elimu nchini.
Alisema
Skuli ya Highlight, ambayo ilianza na kutowa Elimu ya maandalizi katika masomo
ya Sayansi na Lugha, ilianzishwa kwa lengo la kuisaidia Serikali katika kuinuwa
kiwango cha Elimu nchini, ambapo kwa wakati huu imepata maendeleo makubwa
pamoja na changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo.
Hamad
, alieleza hayo huko Chake Chake Pemba, wakati alipokuwa akizungumza na
mwandishi wa habari hizi , juu ya azma ya kuiboresha Skuli hiyo sambamba na
kuanzisha Chuo ambacho kitatowa mafunzo mbali mbali ambayo mbali na Elimu ya
darasani pia itamuwezesha Kijana kuweza kujiajiri.
“
Tunayo azma kubwa mungu akipenda tuanzishe Chuo ambacho kitatowa mafunzo mbali
mbali katika sehemu hii ambayo Skuli hii ipo na baadae Skuli hii tuihamishie katika
eneo letu lililoko Mabaoni Chake Chake , kwa lengo la kuwasaidia Vijana kupata
mafunzo ya fani mbali mbali,” alieleza Mkurugenzi huyo.
Alifahamisha
Skuli hiyo ilianza mwaka 2016 , ikiwa na Wanafunzi 30 wa Nasari pekee ,ambapo
kwa sasa wanao Wanafunzi 120 ambao husoma masomo ya Sayansi na Lugha , na hao walianza
hapo maandalizi hadi Darasa la Kwanza.
Mkurugenzi
huyo, alisema pamoja na mafanikio walioyapata kwa kufanya mahafali ya mwanzo na
kuwawezesha Wanafunzi kuendelea na Darasa la Kwanza hapo, lakini wamekuwa
wakikabiliwa na changamoto mbali mbali kama vile huduma ya Maji Safi na Salama,
Umeme , Vifaa vya kuchezea Wanafunzi wa Nasari na hata Computer.
Kwa
upande wake , Mkuu wa taaluma , Ibrahim Abdulaziz , kwa niaba ya Mwalimu mkuu
wa Skuli hiyo ,alisema lengo la Skuli hiyo ni kwenda mpaka Sekondari kwani
uwezo wa kufanya hivyo kama wataruhusiwa na Wizara utakuwepo hapo baadae
kutokana na Wanafunzi wao kuwa na upeo mzuri.
“
Sisi hatutaishia hapa , lengo letu ni kufikia hatuwa ya Sekondari iwapo tutaruhusiwa
kufanya hivyo , kwani Wanafunzi wetu tumekuwa tukiwaandaa vizuri na maendeleo
yao tunapowapima wanatupa hamasa ya kuwa nao katika Elimu hiyo,” alieleza.
Akizungumzia
suala la mashirikiano baina ya Wazazi , Walimu na Kamati ya Skuli alieleza yapo yakutosha kwani wanapoitwa
hufika kwa wingi na kutowa michango yao ya hali na mali hadi sasa hivi .
Alisema
hadi sasa wanashukuru wazazi wa Watoto wako
bega kwa bega na Walimu hasa
ikizingatiwa Watoto waliopo hapo wengi wao ni wadogo na pale wanapoambiwa
kunahitajika michango wamekuwa wakitekeleza kwa haraka.
Hivyo
wanaomba kuungwa mkono na Serikali yao ili waweze kufikia malengo yao kama
walivyokusudia , kwa kukuza kiwango cha Elimu nchini.
No comments:
Post a Comment