Wachezaji wa Timu ya Yanga, Haji Mwinyi Ngwali na Abdalla Haji "Ninja" wakiwa pamoja na mwandishi wa habari hii Abubakr Khatib "Kisandu" hotelini
Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
MABINGWA wa soka wa Tanzania Bara, Yanga wamewasili kisiwani Unguja leo saa 5 za asubuhi wakitokea Jijini Dar es salam ambapo leo saa 2:00 za usiku watacheza mchezo wa kirafiki na Mlandege SC mchezo ambao utapigwa katika uwanja wa Amaan.
Yanga wamefikia katika Hoteli ya Lail-Noor ambayo ipo Maisara Mjini Unguja.
Kesho asubuhi Yanga wataondoka kisiwani Unguja na kwenda Kisiwani Pemba kuweka kambi kujiandaa na pambano na mtani wake, Simba katika mchezo wa Ngao ya Hisani utakaopigwa Agost 23, 2017 kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es salam.
No comments:
Post a Comment