Habari za Punde

Viongozi wa Dini na Asasi za Kijamii Wapata Elimu ya Sheria na Utayarishaji wa Katiba.

AFISA Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Khalfan Amour Mohamed, akiwaonyesha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar kushoto, washiriki wa mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria, ambao ni viongozi wa dini, asasi za kirai, wanajamii na watu maarufu, mafunzo hayo ya siku mbili, yalifanyika skuli ya Maandalizi Madungu Chakechake Pemba
MWANASHERIA Dhamana kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Pemba, ‘DPP’ Ali Rajab Ali, akiidadavua sheria mpya ya ushahidi ya Zanzibar no 9 ya mwaka 2016, kwa viongozi wa dini, asasi za kirai, wanajamii na watu maarufu, kwenye mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria, yaliofanyika skuli ya Maandalizi Madungu Chakechake, na kutayarishwa na ZLSC tawi la Pemba 
AFISA Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Khalfan Amour Mohamed, akitoa mada ya utayarishaji wa katiba na sheria, kwa viongozi wa dini, asasi za kirai, wanajamii na watu maarufu, mafunzo hayo ya siku mbili, yalifanyika skuli ya Maandalizi Madungu Chakechake Pemba
WASHIRIKI wa mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria, ambao ni viongozi wa dini, asasi za kirai, wanajamii na watu maarufu, kisiwani Pemba wakifuatilia mafunzo hayo ya siku mbili yaliofanyika skuli ya Maandalizi Madungu Chakechake na kuandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.