NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAZAZI na walezi nchini, wametakiwa kutowasafisha
watoto wao waliobakwa au kulawitiwa, na ikitokezea wamewasafisha, wasisite kuwapeleke
hospitali kuwafanyia uchunguuzi, kwani kukosekana kwa maji maji kwenye sehemu
za siri, sio kigezo cha kupoteza ushahidi, makamani.
Kauli hiyo imetolewa na Mwendesha mashitaka kutoka
Afisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kisiwani Pemba, Mohamed Ali Juma wakati
alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa kamati kuu ya mradi wa GEWE, kwenye
mkutano uliofanyika uwanja wa Gombani mjini Chakechake.
Alisema
kukosekana kwa maji maji maalum au mbegu za kiume kwenye sehemu iliofanyiwa
tendo la ulawiti au ubakaji, hakuuwi kesi, kama wengine wanavyofikiria, na wala
ushahidi na ubakaji haondolewi kwa kumuosha mtoto.
Mwendesha
mashiataka huyo, alieleza kuwa hata kama wazazi au walezi watawaosha watoto
wao, waliobakwa au kulawitiwa chamsingi wawafikishe hospitalini, kwa ajili ya
kufanyiwa uchunguuzi wa kitaalamu, na iwapo wamebakwa njia zake za siri
zitaonyesha.
Alifafanua,
tena ni vyema kwa wazazi na walezi hao watawasafisha watoto waliobakwa au
kulawitiwa, ili kuwaepushia na uwezekano wa kukumbwa na magonjwa mbali mbali kama vile ya zinaa.
“Sisi
kesi inapokuja mahakamani za ubakaji, basi daktari anakuja na jawabu kwamba,
ameingiliwa na ipo michubuko au michaniko, lakini marenda, mbegu za kiume, maji
maji yaliotokana na tendo hilo, wala si ushahidi kamili, basi mpenyo ndio
sahihi”,alisema.
Hata
hivyo Mwendesha mashitaka huyo, amesema wananchi kuendelea kutofika mahakamani
kutoa ushahidi kwa sababu ya rushwa muhali, waelewe kuwa ni kuyanaiwirisha
matendo ya udhalilishaji yaliopo nchini.
Kwa
upande wake Afisa Ustawi wa jamii wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed, alisema
bado wasaidizi wa sheria waliopo majimboni, hawajaibuka vya kutosha
kushirikiana na wadau wengine katika mapambano dhidi ya udhalilishaji.
Mratibu
wa wanawake na watoto shehia ya Kangagani Awena Salum Kombo, alisema lazima
iwepo sheria madhubuti ya kuwaadhibu, wasiotaka kufika mahakamani na kutoa
ushahidi.
“Zipo
kesi za udhalilishaji zimesababishwa kufutwa, kwa sababu mtu alieshuhudia au
alieniletea taarifa za awali, hakuwa tayari tena kwenda mahakamni kutoa
ushahidi, lazima kama hawa waadhibiwe”,alifafanua.
Nae
sheha wa shehia ya Mchanga mdogo Asaa Makame Said, alisema kuna ahuweni kubwa
kwenye shehia yake, ikilinganishwa na miaka minne nyuma, kabla ya kufikiwa na
mradi wa kupinga udhalilishaji GEWE.
Kwa
upande wake Mratibu wa mradi wa GEWE (III)
kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar,
Asha Abdi Makame, alisema mradi huo zaidi unakuja kuwajengea uwezo waandishi wa
habari, ili waibue habari zilizofanyiwa utatfiti wa kutosha.
“Tayari
waandishi wameshapewa elimu, na watapita kwenye maeneo yenu, ili kuwauliza na
kutaka takwimu juu ya kesi za udhalilishaji, hivyo wapeni ushirikiano ili
wakamilishe kwa wakati”,alifafanua.
Aidha
Mwenyekiti wa kamati hiyo ya GEWE Khamis Shaban, alisema lazima jamii
waelimishwe, kwamba wasiowaoshe watoto wao waliobakwa au kulawitiwa na
ikitokezea wamewasafisha, wasisite kuwafikisha hospitali kwa kufanyiwa
uchunguzi.
Mradi
wa GEWE III, unatekeleza kwenye wilaya ya Wete kwa Pemba, kwa shehia sita za
Kiungoni, Shengejuu, Mchanga mdogo, Kangagani, Mjini ole na Kinyikani.
No comments:
Post a Comment