STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 23.10.2017
RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia
salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Changwa Lungu kwa
kutimiza miaka 53 tokea Taifa hilo kupata uhuru wake.
Salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana
pamoja na ndugu zao wa Zambia katika kusherehekea siku hii muhimu katika
historia ya nchi hiyo ambapo tukio hili la kihistoria lilitokea Oktoba 24 mwaka
1964 ambapo Zambia ilipata uhuru kutoka koloni la Kiengereza.
Aidha, salamu hizo, zilieleza kuwa tukio hilo
kubwa, linatoa nafasi ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano mkubwa kati ya nchi
mbili hizo hatua ambayo itaimarisha zaidi uhusiano katika nyanja za Kitaifa na
Kimataifa yakiwemo mashirikiano ndani ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini
mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika (AU) pamoja na Jumuiya nyenginezo za
Maendeleo.
Sambamba na hayo, Dk. Shein alimtakia kiongozi
huyo pamoja na familia yake na wananchi wote wa Jamhuri ya Zambia, afya njema
na kuwatakia sherehe njema zenye amani na utulivu wananchi wa nchi hiyo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment